Showing posts with label SIMU ZA MIKONONI. Show all posts
Showing posts with label SIMU ZA MIKONONI. Show all posts

Wednesday, March 16, 2016

WAZIRI PROF. MBARAWA AIPONGEZA TTCL.

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa akisalimiana na wafanyakazi wa TTCL mkoa wa Morogoro. Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa akisalimiana na wafanyakazi wa TTCL mkoa wa Morogoro.Mkuu wa Biasahara Kanda, Nyanda za Juu Kusini Juvenal Utafu akitoa maelezo kuhusu utendaji kazi wa TTCL mbele ya Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa Mkuu wa Biasahara Kanda, Nyanda za Juu Kusini Juvenal Utafu akitoa maelezo kuhusu utendaji kazi wa TTCL mbele ya Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa.Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa akikagua mitambo ya TTCL na Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano mkoa wa Morogoro Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa akikagua mitambo ya TTCL na Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano mkoa wa Morogoro.Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa akikagua mitambo ya TTCL na Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano mkoa wa Morogoro. Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa akikagua mitambo ya TTCL na Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano mkoa wa Morogoro.

 WAZIRI wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mnyaa Mbarawa, ameipongeza Kampuni ya simu TTCL kwa juhudi inazofanya katika kutoa huduma za Mawasiliano nchini na kuitaka kutumia kikamilifu fursa ilizonazo ili kujiendesha kibiashara na kutoa gawio kwa Serikali.

 Waziri Mbarawa ameyasema hayo Mkoani Morogoro Jumatatu hii alipokuwa katika ziara yake ya kukagua kazi zinazofanywa na Taasisi zilizo chini ya Wizara yake na kutoa maelekezo mbalimbali ya kuboresha utendaji wa taasisi hizo. Ziara ya Profesa Mbarawa katika Kampuni ya simu TTCL ilimwezesha kupata taarifa fupi ya utendaji wa Kampuni ya TTCL Mkoa wa Morogoro kwa mwaka 2015 pamoja na mipango na malengo ya Mkoa huo kwa mwaka 2016 ikiwa ni pamoja na mikakati itakayowezesha kuyafikia malengo hayo.

 Aidha Waziri Mbarawa alipata taarifa kuhusu utendaji wa Mkongo wa Taifa wa mawasiliano na changamoto zinazokwamisha Mkongo huo kufanya kazi kwa ufanisi. Uongozi wa TTCL Mkoa wa Morogoro ulimjulisha Waziri Profesa Mbarawa kuwa, kikwazo kikubwa kinachokwamisha utendaji wa Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano uharibifu wa kukatwa kwa mtandao wa Mkongo huo kunakofanywa na baadhi ya wakandarasi wa barabara na wakandarasi wanaojenga mkongo wa kampuni ya simu ya Haloteli pamoja maporomoko ya ardhi huko Njombe na Igavisenga. 

 Akijibu hoja hizo, Profesa Mbarawa aliahidi kushirikiana na Menejimenti na bodi ya TTCL katika kuzifanyia kazi changamoto hizo na kuwataka Wafanyakazi wote kubadilika, kufanya kazi kwa juhudi kubwa na moyo wa uzalendo ili kuiwezesha TTCL kuwa namba moja katika kutoa huduma za Mawasiliano nchini na kumudu ushindani ulipo katika sekta hiyo hivi sasa. Aidha, Waziri Mbarawa aliiagiza Menejimenti ya TTCL kuongeza kasi ya kupanua huduma zote zinazotolewa na kampuni hiyo na hasa Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano ili kukidhi mahitaji makubwa ya huduma hiyo na fursa kubwa ya kibiashara iliyopo kutoka kwa makampuni yanayotoa huduma za tehema.

 Baadhi ya Wafanyakazi wa TTCL walimuuliza Waziri Mbarawa kuhusu tetesi zilizopo kuwa anakusudia kuanzisha taasisi nyingine na kuikabidhi jukumu la kusimamia Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano ambao tangu kuanzishwa kwake, umekuwa chini ya usimamizi wa TTCL ambapo Waziri Mbarawa alikanusha tetesi hizo na kusema kuwa, Serikali ilishafanya uamuzi kwa kuikabidhi TTCL jukumu la kuusimamia na kuuendesha Mkongo wa Taifa wa Mawasiano na hivyo hakuna mpango mwingine tofauti na uamuzi huo. 

 Waziri Mbarawa aliongeza kuwa kuwa, Serikali itaiongezea TTCL jukumu jingine la kusimamia kituo cha kutunzia kumbukumbu (Data Center) kinachotarajia kuanza kazi muda mfupi ujao pamoja na na kuahidi kusaidia kuiwezsha TTCL kupata masafa ili kuongeza uwezo wake wa kutoa huduma.

Friday, October 12, 2012

WADAU WA AIRTEL WAJITOKEZA KUKAGUA MAGARI YAO KWAAJILI YA USALAMA BARABARANI


Askari wa usalama barabarani Meja Anthony Mjema  akikagua gari la mfanyakazi wa Airtel bwana Herald Mwigune wakati Airtel ilipoendeleza juhudu zake za usalama barabarani kwa vitendo kwa kuwezesha magari ya wafanyakazi wake kukaguliwa na kupata sticker za usalama barabarani. Zoezi hilo limefanyika katika makao makuu ya Airtel Morocco.
Askari wa usalama barabarani Meja Anthony Mjema  akikagua gari  wakati Airtel ilipoendeleza juhudu zake za usalama barabarani kwa vitendo na kuwezesha magari ya wafanyakazi wake kukaguliwa na kupata sticker za usalama barabarani. Zoezi hilo limefanyika katika makao makuu ya Airtel Morocco. Pichani Mfanyakazi wa Airtel bwana Herald Mwigune.
Askari wa usalama barabarani Meja Anthony Mjema  akitoa maelezo na ufafanuzi kwa mfanyakazi wa Airtel bi Clara Kizinga juu ya vyombo vya moto wakati wa zoezi la ukaguzi wa magari lililofanyika katika makao makuu ya Airtel Morocco. Zoezi hilo ni mwendelezo wajuhudi za Airtel katika kuhakikisha usalama barabarani unazingatiwa.
Askari wa usalama barabarani Meja Anthony Mjema   akiandika sticker za usalama barabarani mara baada ya kuyakagua magari wakati Airtel ilipoendeleza juhudu zake za usalama barabarani kwa vitendo na kuwezesha magari ya wafanyakazi wake kukaguliwa na kupata sticker za usalama barabarani. Zoezi hilo limefanyika katika makao makuu ya Airtel Morocco. Pichani Mfanyakazi wa Airtel. Pichani ni wafanyakazi wa Airtel Lilian Kibiriti na Abdul Mbuyu
Askari wa usalama barabarani Meja Anthony Mjema   akibandika sticker ya usalama barabarani  katika gari ya mmoja wa wafanyakazi wa Airtel bwana Abadallah Gunda  mara baada ya kukalikagua , hii ni moja kati ya mwendelezo juhudu za Airtel kwa kutekeleza usalama barabarani kwa vitendo na kuwezesha magari ya wafanyakazi wake kukaguliwa. Zoezi hilo limefanyika katika makao makuu ya Airtel Morocco, nyuma ni baadhi ya wafanyakazi wa Airtel wakisubiri kukaguliwa.


Thursday, October 11, 2012

WANAWAKE MKOANI MTWARA WAKABIDHIWA SIMU NA PESA KUPITIA M PESA KWA AJILI YA LISHE



Afisa Elimu Wilaya ya Mtwara Mwl.Mohamed Kahumbi,akionesha aina ya simu iliyowekewa fedha katika akaunti ya M-pesa zinazotolewa bila malipo kwa kwa akina mama wanaonyonyesha kuwawezesha kupokea fedha za kunulnuia chakula chenye lishe kupitia mradi wa Lishe bora na salama wa shirika la mpango wa chakula duniani – WFP. Mradi huo umezinduliwa juzi katika kijiji cha Nanguruwe, Mkoani Mtwara.
Mmoja wa wanufaika wa mradi wa kuwawezesha wanawake wanaonyonyesha na wajawazito mkoani Mtwara kupata chakula chenye lishe akiijaribu simu aliyopatiwa ikiwa na fedha katika akaunti ya M-pesa atakazozitumia kununulia chakula chenye lishe. Fedha na simu hizo hutolewa bila malipo na Shirika la Mpango wa Chakula Duniani – WFP kupitia mradi wake wa Lishe bora na salama.
Afisa Elimu Wilaya ya Mtwara Mwl.Mohamed Kahumbi akimkabidhi simu ya mkononi mmoja wa wanufaika wa mradi wa Shirika la Mpango wa Chakula Duniani – WFP wa kuwapatia fedha wanawake wanaonyonyesha na wajawazito fedha za kununulia chakula chenye lishe kupitia M-pesa wakati wa uzinduzi uliofanyika juzi katika kijiji cah Nanguruwe mkoani Mtwara.
Akina mama wa kijiji cah Nanguruwe mkaoni Mtwara ambao ni wanufaika wa mradi wa Shirika la Mpango wa Chakula Duniani – WFP wa kuwapatia fedha wanawake wanaonyonyesha na wajawazito fedha za kununulia chakula chenye lishe wakijumuika na maofisa wa Vodacom kufurahia simu walizopatiwa zikiwa zimeunganishwa na mtandao wa Vodacom kuwawezesha kupokea fedha za mradi kwa njia ya M-pesa.

Tuesday, October 09, 2012

Airtel yatembelea a watoto wenye mahitaji maalumu wa Uhuru Mchanganyiko




Afisa uhusiano na matukio  wa Airtel  Dangio Kaniki akiwapatia chai watoto shule ya Uhuru Mchanganyiko wakati Airtel ilipotembelea shule hiyo  itakayofaidika na mpango maalumu wa  Airtel kwa kushirikiana na BAMVITA wenye lengo la kuchangia vitabu kwa watoto wenye mahitaji maalum .  Airtel imeanza kutembelea shule zilizopo Dar es Salaam pamoja na mikoani na kubainisha matatizo wanayokumbana nayo ili kuona namna ya kuwasaidia watoto hao wenye mahitaji maalum.

Meneja huduma za jamii wa Airtel Hawa Batuli (katikati)akiongea na mwalimu mkuu wa shule ya Uhuru Mchanganyiko Anna Mang'enya wakati Airtel ilipotembelea shuleni hapo jana. Airtel imeanza kutembelea shule zilizopo Dar es Salaam pamoja na mikoani na kubainisha matatizo wanayokumbana nayo ili kuona namna ya kuwasaidia watoto hao wenye mahitaji maalum.  Kushoto ni Afisa uhusiano na matukio  wa Airtel  Dangio Kaniki

Afisa uhusiano na matukio  wa Airtel  Dangio Kaniki akinywa chai pamoja na watoto wa shule ya Uhuru Mchanganyiko wakati Airtel ilipotembelea shule hiyo  itakayofaidika na mpango maalumu wa  Airtel kwa kushirikiana na BAMVITA wenye lengo la kuchangia vitabu kwa watoto wenye mahitaji maalum .  Airtel imeanza kutembelea shule zilizopo Dar es Salaam pamoja na mikoani na kubainisha matatizo wanayokumbana nayo ili kuona namna ya kuwasaidia watoto hao wenye mahitaji maalum.

Meneja huduma za jamii wa Airtel Hawa Batuli (kushoto) akimshukurua mwalimu mkuu wa shule ya Uhuru Mchanganyiko Anna Mang'enya kwa kuwapokea walipotembelea shule hapo ambapo Airtel imeanza kutembelea shule zilizopo Dar es Salaam pamoja na mikoani na kubainisha matatizo wanayokumbana nayo ili kuona namna ya kuwasaidia watoto hao wenye mahitaji maalum.  Kushoto ni Afisa uhusiano na matukio  wa Airtel  Dangio Kaniki

Story
Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel imewahimiza watanzania kuendelea kuchangia katika mradi wa kuchangia vifaa kwa ajili ya watoto wenye mahitaji maalum unaoendeshwa na Kampuni ya Airtel kwa kushirikiana na  Baraza la maendeleo ya vitabu Tanzania (Bamvita)

Afisa uhusiano na matukio wa Airtel Dangio Kaniki amesema kampuni hiyo ikiwa na Balozi wake, AY imeanza kutembelea shule zilizopo Dar es Salaam pamoja na mikoani na kubainisha matatizo wanayokumbana nayo ili kuona namna ya kuwasaidia watoto hao wenye mahitaji maalum. Airtel inaamini kwamba watoto hao wenye mahitaji maalum wakiwezeshwa kielimu wataweza kutimiza ndoto zao na kuchangia katika maendeleo ya kiuchumi nchini.

Akiongea wakati walipotembelea shuleni hapo Meneja huduma kwa jamii Hawa Bayumi alisema ” Ni matumaini yetu kuwa watanzania na wale wasio watanzania kwa ujumla wataendelea kutuunga mkono ili kuweza kutimiza lengo hili la awali na kisha kuongeza shule za mikoani mara baada ya kukamilisha mahitaji haya katika shule hizi za Dar es Salaam. 

Kampeni hii itaendeshwa kwa muda wa miezi mitatu , na watanzania wanaweza kuchangia kwa kutuma neno “Vitabu”  kwenda namba 15626  na utakuwa umechangia shilingi 200 katika mradi huu au kupitia Airtel Money unapiga *150*60# ingiza jina la biashara VITABU na kuchangia kiwango chochote kile. Tunachukua fulsa hii  kuwaomba  watanzania wote kuchangia ili kuwafikia watoto wengi zaidi nchin”

Nae Mwalimu Mkuu wa shule ya Uhuru Mchanganyiko Anna Mang'enya amesema “shule hiyo inakabiliwa na changamoto mbali mbali ikiwemo uhaba wa vifaa vya kufundishia. bila vifaa hivyo maalum itakuwa vigumu kwa wanafunzi kutimiza ndoto zao zakuendelea kielimu”.

Aidha Ameishukuru Airtel na BAMVITA kwa kuweza kuanzisha mradi huu na kuweza kuwahamasisha watanzania kuchangia ili waweze kupata vitendea kazi  na kuongeza kuwa shule hiyo bado inakabiliwa na changamoto nyingi katika elimu hivyo kuiomba kampuni hiyo kuendelea kuisaidia katika mambo mengine.

  Zena Yahaya Mwanafunzi Uhuru Mchanganyiko alikuwa na haya ya kuongeza “tunawashukuru Airtel kwa kuja kututembelea leo, tunawaomba watanzania wote waendelee kutusaidia kwa kushirikiana na Airtel  katika mradi huu wa Vitabu ili kuweza kutusaidia katika kununua vifaa vya kutusaidia hapa shuleni na kuhakikisha tunapata elimu bora.”

Airtel inatambua umuhimu wa Elimu na tunaamini Tanzania itajengwa na sisi wenyewe hivyo basi lengo la  mradi huu ni kutoa nafasi kwa jamii yetu kuweza kuchangia elimu  ya msingi kwa watoto wenye mahitaji maalum kwa kuwanunulia vitabu na nyenzo za walimu kufundishia. Kwa kuanzia tumeanza kutembelea shule mbili za jijinini Dar es Salaam zitafaidika na mpango huu ambazo ni Sinza Maalum, Uhuru Mchanganyiko ikifuatiwa na Buguruni Viziwi

Friday, September 21, 2012

TIGO KUWEKEZA KWA WAJASIRIAMALI KWA MAISHA BORA YA WATOTO TANZANIA.




 Mkurugenzi mkuu wa Kampuni ya Tigo Tanzania Diego Gutierrez akimkaribisha Waziri wa Maendeleo ya jamii, jinsia na watoto Mh. Sophia Simba kwenye mkutano wa uzinduzi rasmi wa kampeni ya “Tigo Reach for Change” yenye lengo la kuwekeza kwa wajasiriamali watakaotoa mawazo thabiti yatakayosaidia kuboresha maisha ya watoto.

Mkurugenzi mkuu wa Kampuni ya Tigo Tanzania Diego Gutierrez akihutubia wakati wa mkutano huo.
Waziri wa Maendeleo ya jamii, jinsia na watoto Mh. Sophia Simba akimpongeza mkurugenzi mkuu wa Kampuni ya Tigo Tanzania Diego Gutierrez kwa hotuba nzuri aliyoitoa, kulia ni Ofisa wa huduma za jamii wa kampuni ya Tigo Woinde Shisael akipiga makofi.
Waziri wa Maendeleo ya jamii, jinsia na watoto Mh. Sophia Simba akitoa hotuba wakati wa mkutano huo.
Meneja mkuu wa kampuni ya Tigo kitengo cha huduma za jamii , Esther Palsgraaf akihutubia wakati wa uzinduzi rasmi wa kampeni ya “Tigo Reach for Change”.
Wadau na waandishi wa Habari wakifuatilia kwa umakini hotuba iliyokuwa ikitolewa na mkurugenzi wa Tigo Tanzania Diego Gutierrez.
Kampuni ya Simu za mikononi ya Tigo kwa kushirikiana na Taasisi ya Sweden inayojulikana kwa jina la Reach for Change leo wamezindua kampeni ya ‘Tigo Reach for Change’ ambayo imelenga  kuwatafuta na kuwasaidia wajasiriamali wadogo wadogo wenye mawazo imara yatakayosaidia maisha ya watoto Tanzania.
Njia bora ya kuleta mabadiliko ya kijamii ni kwa kuwapatia zana sahihi watu ambao wako tayari kubuni miradi ambayo itaweza kujiendesha yenyewe kwa mda mrefu”alisema Diego Gutierrez,Meneja mkuu wa Tigo Tanzania,tunaamini katika maendeleo na kurudisha sehemu ya kile tunachokipata kwa jamii tunayoihudumia.Tunaamini kila mtoto ana haki ya kuishi maisha kamili na tutawapatia nafasi hiyo katika mradi huu.”aliongeza
Wajasiriamali wenye nia na uwezo wanakaribishwa kuwakilisha mawazo yao kuomba kwa kupitia tovuti ya Tigo au kupeleka mawazo hayo kituo chochote cha huduma kwa wateja cha Tigo. Maombi yote yatapitiwa na jopo la wataalamu na watakaoshinda watajiunga na mpango wa miaka mitatu ambapo mawazo hayo yatabadilishwa na kuwa endelevu kwa kuingia ubia, pia watapata dola za kimarekani 25,000 kila mwaka kwa miaka yote mitatu pamoja na ushauri kutoka wafanyakazi wa ngazi za juu wa Tigo.
Kwa mda ambao mshindi atakuwa akipokea hela kutoka Tigo, mawazo yake yatakuwa yakifanyiwa tathmini ili kuhakikisha kuwa ni bora mpaka hapo mradi utakapoendelezwa na kukamilika.
Kuwajali na kuwapa huduma bora watoto wetu sio jukumu la serikali peke yake”alisema mheshimiwa Sophia Simba waziri wa maendeleo ya jamii, jinsia na watoto.”tunawapongeza Tigo kwa mkakati huu ambao hautasaidia tu maisha ya watoto na vijana Tanzania bali pia itajumuisha kufanya kazi na wajasiriamali wadogo ambao wanakaa ndani ya jamii moja na watoto hao hao,hivyo wanaelewa zaidi matatizo yao.”alisema
Wajasiriamali washindi watatu watatangazwa Desemba mwaka huu na mpango huu utaendelea kwa miaka mitatu, kwa kuchaguliwa washindi watatu kila mwaka.
Reach for change ni Shirika la kujitolea lililopo Sweden ambalo lilianzishwa na Kinnevik,shirika anzilishi la Tigo, Kampeni ya kutafuta wajasiriamali kwa mkakati wa reach for change ulianzia huko Sweden mwaka 2010 ikifuatiwa na Russia 2011 kabla mwaka huo huo kuanzishwa Ghana Afrika ambayo imeweza kuripoti mafanikio makubwa kwa kusaidia kuinua maisha ya watoto zaidi ya 140,000.
Tigo imeanza rasmi utafutaji wa wajasiriamali katika nchi zinazotoa huduma Africa kwa kuzinduliwa kwanza Rwanda ikifuatiwa na Tanzania, Congo DRC,Senegal na mwisho itakuwa Chad.

Thursday, September 20, 2012

TIGO YAMZAWADIA MSHINDI WA PILI NA WA MWISHO WA ‘TIGO BEATS’.

 

Mkazi wa Kijiji cha Kigugu, Kata ya Sungaji, Wilaya ya Mvomero, Mkoa wa Morogoro, Hamis Athuman Pita (19), ( kushoto ) akipokea hundi ya mfano yenye thamani ya shilingi milioni kumi, kwa Msimamizi wa Kampuni ya Tigo Kituo cha Morogoro Neema Mashingia, anayehudumia pia na Mikoa ya Dodoma, Iringa, Mbeya na Ruvuma baada ya kijana hiyo kushinda shindano ya promosheni ya Tigo Beats , iliyoendeshwa na Kampuni hiyo kuanzia Mei 21 hadi Julai 19, mwaka huu, ( kati kati) ni Mfanyakazi wa Tigo Morogoro, Vissa Majitaka.

Tigo imetoa  zawadi kwa mshindi wa pili na wa mwisho  wa droo ya 'Tigo Beats.' Hamisi Athumani kutoka Turiani Morogoro ndiye mshindi wa shilingi 10,000,000/= aliyepatikana wiki iliyopita katika  bahati nasibu  iliyofanyika kwa mfumo wa kompyuta chini ya usimamizi wa Bodi ya Michezo ya Bahati nasibu. 

"Tunajitahidi kutoa huduma bora ambazo tunataka ziboreshe maisha ya wateja wetu," alisema Alice Maro, Afisa uhusiano wa Tigo. "Kwa sababu  ya maendeleo  ya kiteknolojia, tunataka kuwa  pamoja katika maisha ya wateja wetu kila siku na kuwa sehemu ya mafanikio yao," alisema.

Tangu tarehe 21 Mei hadi 19 julai 2012,mteja aliye download  nyimbo yoyote mpya ya Tigobeatz  kwa kuchagua namna mbalimbali za kumwezesha mteja kudownload wimbo kama: kubonyeza alama ya  nyota (*) wakati wanapowapigia ndugu, jamaa au rafiki zao,  kwa kutuma  herufi ya wimbo wowote kwenda 15050, au kwa kupiga 15050 na kununua wimbo wanaoupenda anakuwa tayari amejiingiza katika droo hiyo. Wateja watajiongezea nafasi ya kushinda kwa kila wimbo watakaokuwa wana-udownload.

Tigo inapenda kuwakumbusha wateja wake kutumia  huduma mpya ya 'Tigo Islamic Portal,' kwa ajili ya mwezi huu Mtukufu wa  Mfungo wa Ramadhani. Kwa kupiga namba 0901904444 wateja wa Tigo wataweza  kupata neno katika kitabu cha Koran, Dua,' Hadeeth na Qasida, pamoja na ushauri wa kidini kutoka kwa Shehe. Mteja atatozwa shilingi 0.25/= ili kupata huduma hii kwa mara ya kwanza na kutozwa shilingi 15/= kila siku.

 


Monday, September 17, 2012

MAADHIMISHO YA WIKI YA NENDA KWA USALAMA BARABARANI YANAYODHAMINIWA NA AIRTEL TANZANA KUANZA LEO MKOANI IRINGA



 
Kamanda mkuu kikosi cha usalama barabarani Mohamedi mpinga (Kushoto) akipokea Tshirt kutoka kwa Afisa Uhusiano wa Airtel Jane Matinde zitakazotumika katika maadhimisho ya wiki ya nenda kwa usalama barabarani inayofanyika kitaifa mkoni Iringa ambapo Airtel ni wadhani wakuu. makabithiano hayo yalifanyika katika ofisi za makao makuu ya polisi usalama barabarni jijini Dar es saalam. akishuhudia ni Mkaguzi msaidizi wa polisi inspector Deus Sokoni, madhimisho ya wiki ya Usalama barabarani yanaanza leo jumatatu.
 
Afisa Uhusiano wa Airtel Jane Matinde akizungumza na maasa wa polisi mara baada ya kukabithi Tshirt ambazo zimebeba ujumbe usemao “ Pambana na ajiali za barabarani kwa vitendo, zingatia sheria” zitakazotumika katika maadhimisho ya wiki ya nenda kwa usalama barabarani nchini nzima. Kulia ni Kamanda mkuu kikosi cha usalama barabarani Mohamedi mpinga akifatiwa na Mkaguzi msaidizi wa polisi inspector Deus Sokoni na kushoto ni Mratibu msaidi wa polisi Bonaventura Nsokolo.
 
Mfanyakazi wa Airtel bwana Gregory Ndenyishau akishusha box lenye Tshirts ambazo zitatumika katika wiki usalama barabarani katika ofisi za makoa makuu ya polisi wa usalama barabarani jijini Dar esa saalam ambapo Airtel ni wadhani wakuu wa kampani ya usalam barabarni kwa mwaka huu, akipokea ni Mratibu msaidi wa polisi Bonaventura Nsokolo.

Kampuni ya simu za mikononi ya Airtel imeendeleza dhamira yake ya kushirikiiana na jeshi la polisi usalama barabarani katika kuhakikisha ajali za barabarani zinapungua na kudhibitiwa.

Wiki ya nenda kwa usalama barabarani inafunguliwa kitaifa mkoani Iringa katika viwanja vya Samora kuanzia tarehe 17-22 mwezi Septemba ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa WAZIRI WA MAMBO YA NDANI MHE. DKT. EMMANUEL NCHIMBI kwa niaba ya Mh, Raisi Jakaya Mrisho Kikwete.

akizungumza na wakati wa hafla maalum ya makabidhiano ya Fulana Ofisa Uhusiano wa Airtel Jane Matinde alisema "Airtel tunaona ni haki na ni sawa kuendelea kuthamini usalama barabarni na tunayo dhamira thabiti ya kuhakikisha tunaelimisha na kuhamasisha jamii na waendesha vyombo vya moto kuzingatia na kutii sheria za usalam barabarani, hivyo basi tunaomba watanzania kuunga mkono jitihada hizi ili kuhakikisha kwamba vyombo vya moto zinakaguliwa na kubandikwa stika maalumu za nenda kwa usalama barabarani".

Airtel inadhamini kampeni hii kwa miaka 4 mfululizo ambapo mwaka huu mbali na kuchapisha stickers imejitolea fulana 800 zenye thamani ya Tsh 8 zilizo na ujumbe maalumu kwa mwaka huu usemao“ Pambana na ajali za barabarani kwa vitendo, zingatia sheria” makabidhiano hayo yamefanyika katika ofisi za makao makuu ya polisi usalama barabarini jijini Dar es saalam.

"Airtel Tanzania imeamua kuunga mkono kampeni hii ya nenda kwa usalama barabarani kwa sababu ya ongezeko kubwa la ajali za barabarani ambazo zinaathiri wateja wetu, aliongeza Bi Mtinde.

Bado Airtel haitaishia hapo tayari tumeshajipanga kufanya kampeni mbalimbali zitakazokuwa zikitoa elimu kwa watumiaji wa barabara hasa waenda kwa miguu na madereva wa vyombo vya moto kwa lengo la kupunguza ajali barabarani huku tukishirikiana na jeshi la polisi usalama barabarani. alimaliza kwa kusema.

Nae kamanda Mkuu wa Usalama Barabarani Mohamedi Mpinga alisema "Ninawashukuru sana Airtel kwa ushirikiano wenu katika mkakati wetu wa kupunguza ajali barabarani, hadi sasa maandalizi yote ya wiki ya nenda kwa usalama yamekaa sawa na nawahamasisha sana wananchi wote wajitokeze katika vituo vyetu vyote nchini ili waweze kukagua magari yao na kujipatia stika za usalama barabarani.

Kwa mkoa wa Iringa ambapo ndiko tunafanya maadhimisho ya Usalama barabarani pia tutafanyia ukaguzi pale katika viwanja vya Samora vilevile kituo cha polisi kati maeneo ya sokoni, kituo cha checkpoint ivumbilo na kile cha mafinga, alimaliza kwa kusema Kamanda Mpinga.