Showing posts with label MATUKIO KATIKA PICHA. Show all posts
Showing posts with label MATUKIO KATIKA PICHA. Show all posts

Wednesday, March 16, 2016

KAMATI YA BUNGE YATEMBELEA MAMLAKA YA USIMAMIZI WA BANDARI TANZANIA (TPA), LEO ASUBUHI KUJIONEA SHUGHULI MBALIMBALI ZINAZOFANYWA NA MAMLAKA HIYO

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), Mhandisi Aloyce Matei, akitoa ufafanuzi wa gati zilizo katika bandari hiyo kuhusu kwa Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Miundombinu.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), Mhandisi Aloyce Matei, akitoa ufafanuzi kuhusu namna Kamera zinazoendelea kufungwa katika Bandari hiyo kwa Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Miundombinu, waliotembelea Mamlaka hiyo leo Asubuhi.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), Mhandisi Aloyce Matei, akiwaonyesha Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Miundombinu eneo itakapojengwa gati ya 13 na 14.
Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Kupakia na Kupakua Mizigo Bandarini (TICTS), Paul Wallace akiwaeleza Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Miundombinu namna kampuni hiyo inavyohudumia makontena katika bandari ya Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Sehemu ya Uchukuzi, Dkt. Leornard Chamuriho akitoa taarifa ya namna Wizara inavyosimamia Mamlaka zilizo chini yake,wakati Kamati ya Bunge ya MIundombinu, ilipotembelea Mamlaka ya Bandari(TPA).
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), Mhandisi Aloyce Matei, akifafanua jambo kwa Kamati ya Bunge ya Miundombinu. 

NAIBU WAZIRI DK. KIGWANGALLA ATOA ONYO KALI KWA MADAKTARI NA WAUGUZI WANAOJIHUSISHA NA MATENDO YA KUOMBA NA KUPOKEA RUSHWA

NAIBU Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kigwangalla ametoa onyo kali kwa wanataalum wa sekta ya afya kuacha mara moja vitendo vya kupokea na kuomba rushwa kwani endapo watabainika hatua kali zitachukuliwa dhidi yao.

Dk. Kigwangalla emesema hayo mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam wakati wa ufunguzi wa kuadhimisha siku ya kinywa na meno duniani yaliyofanyika katika viwanja vya shule ya tiba ya kinywa na Meno, Muhimbili.

Ambapo amesema kuwa kwa utawala huu wa sasa Serikali ya awamu ya tano ni dhama nyingine na hawatamvumilia mtu.

“Ninaona tu, bado kuna wachache wanaojihusisha na vitendo vya kuomba rushwa hapa na pale. Kwa dhama hizi ukikutwa hatutakuurumia na hatutamuurumia mtu kwa hili. Tunapaswa kuweka maslai mapana kwa wananchi tunaowahudumia kwenye mioyo yetu” alieleza Dk. Kigwangalla.

Maadhimiho hayo kwa mwaka huu yenye kauli mbiu “Afya njema ya kinywa ni afya ya mwili mzima” kilele chake kinatarajiwa kufikia tamati Mkoani Morogoro ambapo kwa siku zote hizi hadi kilele, Madaktari watatembelea shule maalum kadhaa za ikiwemo ya Mtoni Maalum, Sinza Maalum, Buguruni Maalum na zingine za Mkoa wa Shinyanga na Morogoro ambapo pia watafanya uchunguzi na matibabu ya bure katika siku zote hizo.

Awali katika ufunguzi huo, kulitanguliwa na matembezi maalum ya KM 10, yaliyoongozwa na Naibu Waziri Dk. Kigwangalla ilikuhamasisha afya njema ya kinywa na mwili katika mapambano hayo.
Matembezi maalum ya ufunguzi wa siku ya maadhimisho ya kinywa na meno yaliyofanyika jijini Dar es Salaam yakipita eneo la Maktaba Kuu.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kigwangalla (katikati) aliyeyaongoza matembezi hayo pamoja na viongozi wengine waandamizi akiweo Kaimu Mkurugenzi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, Dk. Maseru (kushoto) na Rais wa Chama cha Madaktari wa Afya ya Kinywa na Meno Tanzania (TDA), Dk. Lorna Carneiro wakiwasili katika viunga vya Eneo la Chuo cha tiba ya meno Muhimbili baada ya kutembea kwa umbali wa KM 10.
Baadhi ya viongozi hao wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kutembea kwa umbali mrefu wa KM 10 kama ishara ya kufungua maadhimisho ya siku ya tiba ya meno duniani.
Rais wa Chama cha Madaktari wa Afya ya Kinywa na Meno Tanzania (TDA), Dk. Lorna Carneiro akisoma hotuba maalum ya ufunguzi huo
Baadhi ya washiriki wakiwa katika mkutano huo
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kigwangalla akitoa hotuba kwa wananchi na wageni waalikwa katika tukio hilo
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kigwangalla akitoa hotuba hiyo.
Mkuu wa Shule ya Kinywa na Meno, DK. Elison Simon akitoa hutuba yake katika tukio hilo.
Baadhi ya wanachama wa Chama cha Madaktari wa Afya ya Kinywa na Meno Tanzania (TDA) wakipata picha ya pamoja na mgeni rasmi, Dk. Hamisi Kingwangalla wakati wa tukio hilo.

Baadhi ya viongozi waandamizi wakiwa katika picha ya pamoja na mgeni rasmi. Kilele cha maadhimisho hayo kinatarajia kufanyika Mkoani Morogoro Machi 20.2016, ambapo watatoa huduma bure ya tiba ya kinywa na meno. (Picha zote na Andrew Chale).

KAMATI YA BUNGE YA MAMBO YA NJE YAKUTANA NA UONGOZI WA WIZARA YA MAMBO YA NJE

Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, Mhe. Balozi Adad Rajab akimkaribisha Naibu Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Mhe. Dkt. Susan Kolimba (hayupo pichani) kuwasilisha taarifa ya Wizara kuhusu Sera, Muundo na Majukumu kwa Wajumbe wa Kamati hiyo. Kikao hicho ambacho kiliwahusisha pia Wakurugenzi kutoka Wizarani kilifanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam tarehe 15 Machi, 2016.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Mhe. Dkt. Susan Kolimba akiwasilisha mada kuhusu Sera, Muundo na Majukumu ya Wizara kwa Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (hawapo pichani)
Sehemu ya Wabunge wakimsikiliza Naibu Waziri alipowasilisha taarifa ya Wizara.
Mkurugenzi wa Chuo cha Diplomasia kilichopo Kurasini Jijini Dar es Salaam, Balozi Mohammed Maundi akiwasilisha taarifa ya utendaji ya Chuo hicho ambacho ni moja ya Taasisi za  Wizara
Wabunge wakifuatilia uwasilishwaji wa taarifa za Wizara
Katibu Mtendaji wa Mpango wa Nchi za Afrika kujitathmini kiutawala Bora (APRM) kwa upande wa Tanzania, Bibi Rehema Twalib akiwasilisha taarifa kuhusu taasisi hiyo ambayo ipo chini ya Wizara ya Mambo ya Nje
Sehemu nyingine ya Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama wakiwa kikaoni
Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC), Bw. Elishilia Kaaya naye akiwasilisha taarifa ya kituo hicho kwa Kamati ya Bunge.
Sehemu ya Wakurugenzi kutoka Wizarani wakifuatilia uwasilishwaji wa taarifa
Wakurugenzi
Baadhi ya Wakurugenzi kutoka Wizarani wakati wa kikao
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Balozi Ramadhan Muombwa Mwinyi akitolea ufafanuzi baadhi ya hoja wakati wa kikao na Kamati ya Bunge
Baadhi ya Wajumbe wa Kamati wakifuatilia.
Sehemu nyingine ya Wakurugenzi wa Wizara
Mkutano ukiendelea
Mhe. Dkt. Kolimba akizungumza na Waandishi wa Habari

RAIS DKT. MAGUFULI AKAGUA NA KUWEKA JIWE LA MSINGI KATIKA UJENZI WA KITUO CHA KUFUA UMEME CHA KINYEREZI II JIJINI DAR.

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Balozi wa Japan nchini Masaharu Yoshida, Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo, Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Dar es Salaam CCM, Ramadhan Madabida, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya  Nishati na Madini Dkt. Juliana Palangyo wakikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa Ujenzi wa Kituo cha Kufua umeme cha Kinyerezi II nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Balozi wa Japan nchini Masaharu Yoshida , Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo, Mkurugenzi mkuu wa Tanesco Felchesmi Mramba wakivuta utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa Ujenzi wa Kituo cha Kufua umeme cha Kinyerezi II nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam.
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisikiliza maelezo kutoka Meneja wa Kituo cha kufua umeme cha Kinyerezi I Mhandisi John Mageni kuhusu utendaji kazi wa kituo hicho.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akianza ukaguzi katika Mitambo ya kuzalisha umeme ya Kinyerezi I nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akitoa maelekezo kwa Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo kuhusu ujenzi wa Kituo cha Kufua umeme cha Kinyerezi I nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam.
  Meneja wa Kituo cha kufua umeme cha Kinyerezi I Mhandisi John Mageni akitoa maelekezo kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kuhusu mitambo ya kufua umeme kwa kinyerezi I nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam.
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wananchi wa kinyerezi hawapo pichani kabla ya kuzindua rasmi Ujenzi wa Kituo cha Kufua umeme cha Kinyerezi II nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam.
  Mkurugenzi mkuu wa Tanesco Felchesmi Mramba akifafanua jinsi ujenzi wa Kituo cha kufua umeme cha Kinyerezi II kitakavyokuwa mara baada ya kukamilika  mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda .
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia jambo na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Dar es Salaam CCM Ramadhani Madabida kabla ya uzinduzi wa uzinduzi rasmi wa Ujenzi wa Kituo cha Kufua umeme cha Kinyerezi II nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo, Balozi wa Japan Nchini Masaharu Yoshida, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda , Mama Janeth Magufuli wakiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa TANESCO mara baada ya kuzindua rasmi ujenzi  wa Kituo cha Kufua umeme cha Kinyerezi II nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam.
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimsikiliza kwa makini mama mmoja alijitokeza kumpongeza kutokana na utendaji kazi mzuri wa Serikali yake ya awamu ya tano mara baada ya uzinduzi rasmi ujenzi wa wa Kituo cha Kufua umeme cha Kinyerezi II nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam.
Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo akimkaribisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli wakati alipowasili kwenye ofisi za kituo cha kuzalisha umeme cha Kinyerezi I nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam.
 Wananchi wakishangilia wakati Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli alipokuwa akiwahutubia huko Kinyerezi nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam. 
PICHA NA IKULU

SIKU YA UTEPE MWEUPE WA UZAZI SALAMA YAADHIMISHWA JIJINI DAR ES SALAAM LEO.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Hassan Suluhu akizungumza wakati wa siku ya Utepe Mweupe ambapo na uzinduzi wa kampeni ya kuzuia vifo vya mama na mtoto katika mkutano uliofanyika katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam leo.
Pia mama Samia amewasihi wanawake kujiunga na mfuko wa jamii wa bima ya afya ili kusaidia vituo vya afya. Pia amewataka wananchi kuachana na mila potofu hasa za ukeketaji kwani ni kumkosoa mwenyezi Mwenyezi Mungu. 
Mganga Mkuu wa Serikali, Profesa Mohamed Bakari Kambi akizungumza wakati wa kuadhimisha siku ya Upete Mweupo kwa niaba ya Waziri wa Afya maendeleo ya jamii, Jinsia, wazeee na watoto, Ummy Mwalimu leo katika uzinduzi wa kampeni ya kuzuia vifo vya mama na mtoto katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam leo.
Mwakilishi wa UNICEF akizungumza wakati wa kuadhimisha siku ya Utepe mweupe  ambapo mama Samia amezindua wa kampeni ya kuzuia vifo vya mama na mtoto amesema atashirikiana vyema katika kuzuia vifo vya watoto wakati wa kuzaliwa.
 Mwakilishi wa mganga mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Benedict Msiba  akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni ya kuzuia vifo vya  mama na mtoto wakati wa kujifungua, ikiwa amesema kuwa katika mkoa wa Rukwa umejitahidi kupunguza vifo vya mama na mtoto wakati wa kujifungua.
 shuhuda, Efrazia Saidia ambaye amenusurika kifo cha chake na mwanae kutokana na kuumwa uchungu kwa muda mrefu.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Hassan Suluhu akionyesha vitabu ambavyo vimezinduliwa leo ambayo ni mpango wa serikali kuendelea  kuchangia  kupunguza vifo vya mama na mtoto.
 

Baadhi ya wananchi waliojitokeza katika siku ya Utepe mweupe jijini Dar es Salaam leo na uzinduzi wa mpango mkakati wa kuzuia vifo vya mama na mtoto wakati wa kujifungua.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Hassan Suluhu akiwa katika picha ya pamoja na kamati ya maandalizi  wa siku ya Utepe Mweupe leo jijini Dar es Salaam.
Picha na Avila Kakingo, Globu ya Jamii.