Monday, October 06, 2014

Airtel yazindua Mashindano ya kuvumbua vipaji vya Muziki


Airtel yazindua Mashindano ya kuvumbua vipaji vya Muziki

Mkurugenzi wa kitengo cha Masoko wa Airtel Levi Nyakundi akiongea wakati wa uzinduzi wa mashindano ya kusaka vipaji kupitia simu ya mkononi yajulikanayo kama " Airtel TRACE Music Star" kwa lengo la kukuza na kuvumbua vipaji vya wana muziki chipukizi na kuwawezesha kufikia ndoto zao. Program hii ni kwa ushirikiano kati ya Airtel, kampuni ya Trace pamoja na Mwanamuziki wa Marekani Akon, uzinduzi huo ulifanyika mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa high spirit - IT Plaza jijini Dar es saalam.


Meneja Masoko wa Airtel Bi Aneth Muga akiongea wakati wa Uzinduzi wa program ya Airtel Trace Music Star , program itakayowawezesha wanamuziki chipukizi kuonyesha vipaji vyao vya muziki kwa kupitia simu zao za mkononi.

Mwanamuziki wa Bongo Flava Ommy Dimples akitumbuiza wakati wa uzinduzi wa mashindano ya kusaka vipaji kupitia simu ya mkononi yajulikanayo kama " Airtel TRACE Music Star"kwa lengo la kukuza na kuvumbua vipaji vya wana muziki chipukizi na kuwawezesha kufikia ndoto zao. Program hii ni kwa ushirikiano kati ya Airtel, kampuni ya Trace pamoja na Mwanamuziki wa Marekani Akon. uzinduzi huo ulifanyika mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa high spirit - IT Plaza jijini Dar es saalam

Mkurugenzi Mkuu wa Airtel Tanzania Sunil Colaso (kulia) akifatilia kwa karibu uzinduzi wa program ya kusaka vipaji vya muziki ijulikanayo kama Airtel Trace Music Star.
Meneja Uhusiano wa Airtel Bwana Jackson Mmbando akiwa na msaani wa muziki wa kizazi kipya Lady JD wakati wa uzinduzi wa Airtel Trace Music Star.