Tuesday, March 29, 2016

Mbunifu wa mavazi Jocktan Makeke awakilisha Tanzania katika Maonyesho ya Mavazi ya Afrika Mashariki (East Africa Fashion Week) jijini Nairobi


Mbunifu wa mavazi Jocktan Makeke awakilisha Tanzania katika Maonyesho ya Mavazi ya Afrika Mashariki (East Africa Fashion Week) jijini Nairobi
Mbunifu wa mavazi Jocktan Makeke (kati) akiwakilisha Tanzania jana tarehe 26 March 2016 kwenye hotel ya Boma Inn Nairobi. Maonesho haya makubwa ya mitindo yamejumuisha nchi mwanachama wa Afrika Mashariki yaani Tanzania, Kenya, Rwanda, Burundi, Uganda na Sudan ya Kusini.
Makeke kaenda kuiwakilisha collection  yake inaitwa THE AFRICAN BEAUTY IN THE DARKNESS - TABID, au uzuri wa Afrika gizani  kwa Kiswahili,  giza inawakilisha utamaduni wa Magharibi ambao kwa sasa umekua kwa kasi mno katika bara la Afrika na kutufanya waafrika kusahau utamaduni wetu. 
Lakini licha ya kuzungukwa na hili giza zito la umagharibi lakin bado Afrika inameremeta kwani kuna tamaduni zetu nzuri ambazo zinafaa kuigwa duniani kote. Makeke ametumia malighafi za asili kutengeneza mavazi yake na nakshi asili za kiafrika. 
 Vazi lililobuniwa na Mbunifu wa mavazi Jocktan Makeke kutoka Tanzania kwenye maonesho hayo

 Collection ingine ya mbunifu wa mavazi Jocktan Makeke kutoka Tanzania 
Ubunifu wa makeke