Friday, July 04, 2014

WAANDISHI KUNOLEWA VITA DHIDI YA UPANGAJI MATOKEO



WAANDISHI KUNOLEWA VITA DHIDI YA UPANGAJI MATOKEO
waandishi+wa+habariNa Boniface Wambura, Dar es salaam
Taasisi moja kutoka Uingereza inayohusika na kampeni dhidi ya upangaji matokeo kwenye mpira wa miguu (match fixing) itafanya uwasilishaji (presentation) juu ya suala hilo kwa waandishi wa habari za michezo nchini.

 Uwasilishaji huo utafanyika kesho (Julai 5 mwaka huu) saa 11 jioni kwenye hoteli ya Accomondia iliyopo Barabara Nkrumah jijini Dar es Salaam.
 Wataalamu hao wa kupiga vita upangaji matokeo ambao pia wataelezea jinsi matokeo yanavyopangwa, jana (Julai 3 mwaka huu) walifanya uwasilishaji wao kwa wachezaji na benchi la ufundi la timu ya Taifa ya vijana wenye umri chini ya miaka 17 (Serengeti Boys).
 Taasisi hiyo yenye kibali kutoka Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) katika utoaji elimu ya kubaini upangaji matokeo, vilevile inatoa elimu juu ya athari zinazopatikana kutokana na upangaji matokeo.