Monday, September 17, 2012

MWAKYEMBE ZIARANI BERLIN, Ujerumani


Waziri wa uchukuzi Dkt. Harrison Mwakyembe na ujumbe wake wapo Berlin kuanzia  15 hadi 19 sept, 2012 kwa ziara ya kikazi. Moja ya matukio muhimu ni kusainiwa Mkataba wa Ushirikiano wa Usafiri wa Anga (Bilateral Air Services Agreement - BASA) baina ya nchi hizi mbili tarehe 17 Sept. Aidha, tarehe 16 sept, Mhe. Waziri na ujumbe wake walitembelea maonyesho ya Kimaitaifa ya sekta ya Usafiri wa Anga yaliofanyika jijini Berlin ambapo  kwa nyakati mbalimbali, Mhe. na ujumbe wake wanakutana na wafanyabiasha na wawekezaji mbalimbali hususani katika sekta ya usafiri wa anga, reli na majini.

 
 Mhe. Waziri akiwa ndani ya moja ya ndege iliyokuwepo katika maonyesho hayo.
 
 Mhe. Waziri akipata maelezo kutoka kwa mtaalamu wa ndege za Airbus, nchini ujeruman (hayupo pichani) pembeni yake ni Mhe. balozi wa tz Berlin.
 
 mhe. waziri akiwa na Balozi wa tz Berlin Mhe. Ahmada R. Ngemera (kushoto) na Afisa wa Wizara ya mambo ya Nje, Ali Ubwa Mussa (Kulia).
 
  Mhe. Waziri na ujumbe wake wakiwa katika maonyesho ya Sekta ya usafiri wa Anga mjini Berlin.
 
Mhe. Waziri na ujumbe wake wakiwa katika Majadiliano na Uongozi wa Sekta ya Usafiri wa Anga, Germany.