Sunday, March 29, 2015

ZITTO ACHAGULIWA KUIONGOZA ACT-TANZANIA



ZITTO ACHAGULIWA KUIONGOZA ACT-TANZANIA Kiongozi mpya wa chama cha ACT Tanzania Zitto Kabwe, akilakiwa na wajumbe wa mkutano mkuu wa chama hicho, wakati wa uchaguzi mkuu uliofanyika kwenye ukumbi wa Kadinali Rugambwa, Oysterbay jijini Dar es Salaam, Jumamosi Machi 228, 2015. 

Zitto alichaguliwa kuwa kiongozi wa chama hicho nafasi ambayo kwa katiba ya chama hicho ndiyo ya juu zaidi. Nafasi zingine ni Mwenyekiti wa chama, namakamu wake, wa Tanzania visiwani na Tanzania bara, hali kadhalika nafasi ya ukatibu mkuu na manaibu wake wiwili. 

Chama hicho kitazinduliwa rasmi Jumapili kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee Hall jijini Dar es Salaam.
Zitto akionyesha alama ya chama ambayo ni "Uwazi".

                Zitto akihutubia wajumben wakati wa uchaguzi huo.

       Wajumbe wakifurahi kwa kushikana mikono kuonyesha umoja.
                                Wajumbe wakipiga kura.
Aliyekuwa katibu mkuu wa muda wa ACT-Tanzania, Samson Mwigamba, akihutubia.


Msimamizi wa uchaguzi huo, Profesa Kitila Mkumbo.