Thursday, March 26, 2015

NAFASI 56 ZA AJIRA SERIKALINI.



NAFASI 56 ZA AJIRA SERIKALINI.

(Barua zote ziandikwe kwa Mkurugenzi Mtendaji Wilaya)
TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga anakaribisha maombi ya kazi kwa Wananchi wenye sifa za kujaza nafasi za kazi kama ifuatavyo



NAFASI: KATIBU MAHSUSI DARAJA LA III (Nafasi 5)
Sifa
• Awe amehitimu kidato cha nne na kuhudhuria mafunzo ya Uhazili na kufaulu hatua ya tatu
• Awe amefaulu somo la hatimkato ya Kiswahili na Kiingereza maneno 80 kwa dakika
• Awe amepata mafunzo ya kompyuta kutoka chuo chochote kinachotambuliwa na serikali na kupata cheti katika program za Windows, Microsoft office, Internent, Email and Publisher
Ngazi ya mshahara
TGS B 345,000 Hadi 428,700 kwa mwezi
Kazi na Majukumu
• Kuchapa barua, taarifa na nyaraka za kawaida
• Kusaidia kupokea wageni na kuwasaili shida zao, na kuwaelelekeza sehemu wanapoweza kushughulikiwa
• Kusaidia kutunza taarifa/kumbukumbu za matukio, miadu ya wageni, tarehe za vikao, safari za Mkuu wake na ratiba ya kazi zingine zilizopangwa kutekelezwa katika ofisi anamofanyia kazi, na kumtaarifu Mkuu wake kwa wakati unaohitajika
• Kusaidia kutafuta na kumpatia Mkuu wake majalada, nyaraka na kitu chochote kinachohitajika katika shughuli za kazi hapo ofisini
• Kusaidia kufikisha maelekezo ya Mkuu wake wa kazi kwa wasaidizi wake na pia kumwarifu kuhusu taarifa zozote anazokuwa amepewa na wasaidizi wake
• Kusaidia kupokea majalada, kuyagawa kwa maofisa walio katika sehemu alipo na kuyakusanya, kuyatunza na kuyarudisha sehemu zinazohusika
• Kutekeleza kazi zozote atakazokuwa amepangiwa na msimamizi wake wa kazi
UTARATIBU WA KUTUMA MAOMBI
• Barua za maombi ziandikwe kwa mkono
• Barua za maombi ziambatanishwe na nakala/vivuli vya vyeti vya Elimu na ujuzi pawe na taarifa binafsi (CV)
• Waliojiriwa wapitishe maombi yao kwa waajiri wao wa sasa
• Barua ya maombi iwe na anuani ya kuaminika na ikiwezekana na simu au namba ya fax
• Weka picha passport size (2)
Barua zitumwe kwa
Mkurugenzi Mtendaji (W)
S.L.P 194
MBINGA
Mwisho wa kupokea maombi ni tar 31/03/2015
Hussein N. Issa
MKURUGENZI MTENDAJI (W)
MBINGA
Source: Habari Leo 25th March 2015
============
HALMASHAURI YA WILAYA YA MBINGA
(Barua zote ziandikwe kwa Mkurugenzi Mtendaji Wilaya)
TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga anakaribisha maombi ya kazi kwa Wananchi wenye sifa za kujaza nafasi za kazi kama ifuatavyo
NAFASI: AFISA MTENDAJI KIJIJI DARAJA LA III (Nafasi 35)
Sifa
Awe amehitimu wa kidato cha IV na kupata mafunzo ya Astashahada/Cheti katika moja ya fani zifuatazo
i. Utawala
ii. Sharia
iii. Elimu ya Jamii
iv. Msimamizi wa fedha
v. Maendeleo ya jamii sayansi na sanaa kutoka Chuo cha Seriakali za Mitaa Hombolo-Dodoma au chuo chochote kinachotambuliwa na serikali
Ngazi ya Mshahara: TGS B S345,000 Hadi 428,000 kwa mwezi
Kazi na Majukumu
• Afisa Masuulin na Mtendaji Mkuu wa Serikali ya Kijiji
• Mlinzi wa Amani na Msimamizi wa Utawala Bora katika Kijiji
• Kuratibu na kusimamia upangaji wa utekelezaji wa Mipango ya Maendeleo ya Kijiji
• Katibu wa Mikutano na kamati zote za Halmashauri ya Kijiji
• Kutafsiri na Kusimamia Sera, Sheria na Taratibu
• Kusimamia, kukusanya na kutunza kumbukumbu zote na nyaraka za kijiji
• Kiongozi wa Wakuu wa Vitengo vya Kitaalamu katika Kijiji
UTARATIBU WA KUTUMA MAOMBI
• Barua za maombi ziandikwe kwa mkono
• Barua za maombi ziambatanishwe na nakala/vivuli vya vyeti vya Elimu na ujuzi pawe na taarifa binafsi (CV)
• Waliojiriwa wapitishe maombi yao kwa waajiri wao wa sasa
• Barua ya maombi iwe na anuani ya kuaminika na ikiwezekana na simu au namba ya fax
• Weka picha passport size (2)
Barua zitumwe kwa
Mkurugenzi Mtendaji (W)
S.L.P 194
MBINGA
Mwisho wa kupokea maombi ni tar 31/03/2015
Hussein N. Issa
MKURUGENZI MTENDAJI (W)
MBINGA
Source: Habari Leo 25th March 2015
============
HALMASHAURI YA WILAYA YA MBINGA
(Barua zote ziandikwe kwa Mkurugenzi Mtendaji Wilaya)
TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga anakaribisha maombi ya kazi kwa Wananchi wenye sifa za kujaza nafasi za kazi kama ifuatavyo
NAFASI: AFISA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU II (Nafasi 4)
Sifa
Awe amehitimu kidato cha nne (IV) na kupata mafunzo ya utunzaji wa kumbukumbu katika moja ya fani za Afya masjala, Mahakam na Ardhi katika ngazi ya Astashahada/Cheti
Ngazi ya Mshahara:
TGS B 345,000 Hadi 428,700 kwa mwezi
kazi na Majukumu
(i) Kutafuta kumbukumbu/nyaraka/mafaili yanayohitajiwa na wasomaji
(ii) Kudhibiti upokeaji uandikishaji wa kumbukumbu/nyaraka
(iii) Kuchambua, kuorodhesha na kupanga kumbukumbu/nyaraka
(iv) Kuweka/kupanga kumbukumbu/nyaraka katika masjala
(v) Kushughulikia maombi ya kumbukumbu/nyaraka kutoka taasisi za serikali
UTARATIBU WA KUTUMA MAOMBI
• Barua za maombi ziandikwe kwa mkono
• Barua za maombi ziambatanishwe na nakala/vivuli vya vyeti vya Elimu na ujuzi pawe na taarifa binafsi (CV)
• Waliojiriwa wapitishe maombi yao kwa waajiri wao wa sasa
• Barua ya maombi iwe na anuani ya kuaminika na ikiwezekana na simu au namba ya fax
• Weka picha passport size (2)
Barua zitumwe kwa
Mkurugenzi Mtendaji (W)
S.L.P 194
MBINGA
Mwisho wa kupokea maombi ni tar 31/03/2015
Hussein N. Issa
MKURUGENZI MTENDAJI (W)
MBINGA
Source: Habari Leo 25th March 2015
============
HALMASHAURI YA WILAYA YA MBINGA
(Barua zote ziandikwe kwa Mkurugenzi Mtendaji Wilaya)
TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga anakaribisha maombi ya kazi kwa Wananchi wenye sifa za kujaza nafasi za kazi kama ifuatavyo
NAFASI: AFISA MAENDELEO YA JAMII MSAIDIZI SADARA LA II (Nafasi 12)
Wenye elimu ya kidato cha IV waliohitimu mafunzo ya Astashada/Cheti katika fani ya Maendeleo ya Jamii kutoka chuo chochote kinachotambuliwa na Serikali
TGS B 345,000 Hadi 428,700 kwa mwezi
Kazi na Majukumu
• Kuratibu shughuli za maendeleo ya Jamii katika kijiji zikiwemo za watoto na kusingatia jinsia
• Kuwezesha jamii kushiriki katika kubuni, kupanga kutekeleza, kusimamia kutathimini mipango/miradi ya maendeleo
• Kuhamasisha na kuawezesha wananchi kupanga na kutekeleza kazi za maendeleo ambazo ni pamoja na usafi wa mazingira, ujenzi wa nyumba bora vijijini, ujenzi wa shule, Zahanati, Majosho, barabara za vijiji (feader roads) uchimbaji majosho, visima vifupi na uchimbaji wa marambo
• Kuhamasisha na kuwawezesha wananchi kupanga mbinu za kutatua vikwazo vya maendeleo hasa vya maji na nishati kwa kuwa na miradi ya uvunaji maji ya mvua, majiko na matumizi ya mikokokteni
• Kutoa na kuwezesha upatikanaji wa mafunzo kwa viongozi wa kijiji na vikundi mbalimbali vya maendeleo kijijini kuhusu
(a) Utawala bora na uongozi
(b) Ujasiriamali
(c) Mbinu shirikishi jamii na kazi za kujitegemea
(d) Chakula bora na lishe
(e) Utunzaji na malezi bora ya watoto
• Kuwa kiungo kati ya wanakijiji (Afisa Mtendaji wa Kata) na watu wengine wa serikali katika kutekeleza shughuli za maendeleo
• Kuwawezesha ananchi kupanga na kutekeleza kazi za kujitegemea
Sifa za Jumla za mwombaji awe
• Raia wa Tanzania
• Hajawahi kuajiriwa na kufukuzwa/kustaafu kazi
• Hajawahi kuhusika na makosa ya jinai
• Umri usiozidi miaka 40
• Awe na wadhamini wawili wa kuaminika
UTARATIBU WA KUTUMA MAOMBI
• Barua za maombi ziandikwe kwa mkono
• Barua za maombi ziambatanishwe na nakala/vivuli vya vyeti vya Elimu na ujuzi pawe na taarifa binafsi (CV)
• Waliojiriwa wapitishe maombi yao kwa waajiri wao wa sasa
• Barua ya maombi iwe na anuani ya kuaminika na ikiwezekana na simu au namba ya fax
• Weka picha passport size (2)
Barua zitumwe kwa
Mkurugenzi Mtendaji (W)
S.L.P 194
MBINGA
Mwisho wa kupokea maombi ni tar 31/03/2015
Hussein N. Issa
MKURUGENZI MTENDAJI (W)
MBINGA
Source: Habari Leo 25th March 2015