Monday, October 06, 2014

Waziri wa Mazingira afanya ziara ya kukagua viwanda mbalimbali jijini Dar leo



Waziri wa Mazingira afanya ziara ya kukagua viwanda mbalimbali jijini Dar leo
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais - Mazingira Dkt. Eng. Binilith Satano Mahenge (wa kwanza kushoto,) akiwa pamoja na Mkurugenzi Msaidizi Ofisi ya Makamu wa Rais Magdalena Mtenga,(mwenye nguo nyekundu) na Dr. Robert Ntakamalenga, Mkurugenzi wa Uzingatiaji na Utekelezaji-NEMC katika ziara ya kukagua viwanda jijini Dar Es Salaama leo.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais - Mazingira Dkt. Eng. Binilith Satano Mahenge, akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Kiwanda cha Bin Fijaa Industry Bwana Ahmed Abdallah, jinsi wanavyo tumia mashine na maligafi mbalimbali katika kuzalisha mifuko. Kiwanda hiko kipo barabara ya Nyerer jijini Dar Es Salaam.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais - Mazingira Dkt. Eng. Binilith Satano Mahenge, akikagua mifuko inayozalishwa na kiwanda cha Tanplast Ltd anayemuonyesha Waziri mifuko hiyo ni Bwana Kaushal Josh ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kiwanda hicho.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais - Mazingira Dkt. Eng. Binilith Satano, akizungumza na Waandishi wa habari baada ya kuhitimisha ziara yake ya kukagua viwanda mbalimbali vya jijini Dar Es Salaam.