Friday, August 08, 2014

Katibu Mkuu kiongozi katika maonyesho ya Nane nane kanda ya kati Dodoma


Katibu Mkuu kiongozi katika maonyesho ya Nane nane kanda ya kati Dodoma
Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue akisalimiana na wafanyakazi waliopo katika maonyesho ya Nane nane katika Jengo la maonyesho la Ofisi ya Rais maeneo ya Nzuguni Dodoma ambapo maonyesho haya yameadhimishwa kwa kushirikisha mikoa ya kanda ya kati.
Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue akiangalia baadhi ya Bidhaa zinazotengenezwa na badhi ya wajasiriamali wanaonufaika na mfuko wa maendeleo ya jamii-TASAF (Tanzania Social Action Fund) ndani ya Jengo lamaonyesho la Ofisi ya Rais Nzuguni Dodoma.
Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue akisaini kitabu cha wageni katika Jengo la maonesho la ofisi ya Rais.
Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue katikati akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi waliopo katika jingo la maonyesho nane nane 2014 Ofisi ya Rais Nzuguni Dodoma. Picha na Deusdedit Moshi wa Michuzi Blog Kanda ya kati.