Saturday, May 31, 2014

Wafanyakazi wa Benki ya NBC waipiga jeki timu ya watoto wenye ulemavu wa akili Zanzibar




Wafanyakazi wa Benki ya NBC waipiga jeki timu ya watoto wenye ulemavu wa akili Zanzibar
 Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Balozi Seif Ali Idd (kulia) akipokea  msaada wa sh milioni mbili kutoka kwa Meneja wa NBC tawi la Zanzibar, Rajab Maalim (kushoto) zilizochangwa na wafanyakazi wa benki hiyo kwa ajili ya timu ya watoto wenye  ulemavu wa akili watakaoshiriki michezo ya olimpiki maalumu inayotarajiwa kuanza Juni 6 mwaka huu Wilayani Kibaha katika Mkoa wa Pwani. makabidhiano yalifanyika kwenye ofisi za makamu wa rais, Vuga, Zanzibar jana
 Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, : Balozi Seif Ali Idd akikabidhi fedha zilizochangwa na wafanyakazi wa NBC nchini pamoja na yeye mwenyewe kwa  Makamu Mwenyekiti wa Kamati Maalumu ya Olimpiki Zanzibar, Saada Hamad katika hafla hiyo mjini Zanzibar.
Baadhi ya watoto wenye ulemavu wa akili watakaoshiriki michuano hiyo  wakiwa katika hafla hiyo.