Saturday, May 31, 2014

Bunge lapitisha Bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini kwa Mwaka 2014/2015



Bunge lapitisha Bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini kwa Mwaka 2014/2015
 Waziri Mkuu Mhe.Mizengo Pinda kushoto akiwa amempa mkono Naibu Waziri wa Nishati na Madini Mhe Stephen Masele wakati akimpongeza mara baada ya Bunge kupitisha Bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini kwa Mwaka 2014/2015.
 Waziri Mkuu Mhe.Mizengo Pinda katikati akiwa akiwa ameshikana mikono  na Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini Bw.Eliakim Maswi na  Naibu Waziri wa Nishati na Madini Mhe Stephen Masele wakati akiwapongeza mara baada ya Bunge kupitisha Bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini kwa Mwaka 2014/2015.
 Waziri wa zamani wa nishati na Madini Mhe.William Ngeleja kulia akimpongeza Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini Bw.Eliakim Maswi 
 Waziri Mkuu Mhe.Mizengo Pinda  katikati akiwa katika picha ya pamoja na familia ya Waziri wa Nishati na Madini Mhe.Prof.Sospeter Muhongo mara baada ya Bunge kupitisha Bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini kwa Mwaka 2014/2015.
  Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini Bw.Eliakim Maswi akitoka katia ukumbi wa Bunge akiwa ameongozana na baadhi ya wabunge kutoka kushoto,Mhe.Mustafa Mkullo,Lucy Mayenga,Mhe.Rdhiwani Kikwete na Mh.Abuu Jumaa mara baada ya Bunge kupitisha Bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini kwa Mwaka 2014/2015.
Na Deusdedit Moshi  Mtendaji Mkuu wa Photo Solutions wawakilishi wa Michuzi Blog Kanda ya Kati.