Tuesday, September 25, 2012

Mwandishi wa Habari wa Tanzania Daima Agness Yamo Afariki Dunia



Mwandishi wa Habari wa Tanzania Daima Agness Yamo (pichani) amefariki dunia. 
---
Habari zilizotufikia zinasema Agness Yamo amefariki leo Sept 25, 2012 katika Hospitali ya Jeshi Lugalo alikokuwa akipatiwa matibabu baada ya kuugua kwa muda mfupi.

Mipango ya mazishi inafanyika nyumbani kwa kakayake Buguruni Sokoni katika Magorofa ya Muhimbili. Marehemu alizaliwa 8/8/1978 na katika uhai wake alifanya kazi katika makampuni mbalimbali ya magazeti na hadi mauti yanamfika alikuwa Mwandishi wa gazeti la Tanzania Daima.

  HakingowiBlog, inatoa pole kwa Ndugu, Jamaa na marafiki wote pamoja na Uongozi wa Free Media kwa msiba huo uliowafika. 
Mungu aipe pumziko la amani roho ya marehemu Agness Yamo, AMINA.