WIZARA YA AFYA NA USTAWI WA JAMII Kwa kushirikiana na TAASISI YA BENJAMIN WILLIAM MKAPA HIV/AIDS
TANGAZO LA KAZI
Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kwa kushirikiana na Taasisi ya Benjamin William Mkapa HIV/AIDS inatekeleza Mradi wa kuimarisha mifumo ya huduma za afya ( Health Systems Strengthening) kupitia ufadhili wa Mfuko wa Duniawa kupambana na UKIMWI, Kifua Kikuu na Malaria - Mzunguko wa 9 ( Global Fund Round 9). Baadhi ya malengo ya mradi ni pamoja na; kuongeza wataalam wa afya, ili kuimarisha huduma za UKIMWI, Kifua Kikuu, Malaria na huduma nyinginezo, katika Halmashauri zilizopo maeneo yenye uhaba mkubwa wa watumishi kutokana na changamoto ya mazingira yake.
Baadhi ya malengo ya mradi ni pamoja na kuimarisha uwezo wa vyuo vya mafunzo ya afya, kwa kuvipatia wakufunzi zaidi, ili kuhakikisha kuwa uzalishaji wa wataalam wa afya unaongezeka zaidi nchini. Katika kutekeleza azma hii, BMAF wanatoa tangazo la nafasi za kazi kwa waalimu 137 wa vyuo vya Afya, kama ifuatavyo:
KANDA YA KATI (CENTRAL ZONE) | ||
CHUO | KADA | IDADI |
i. MIREMBE School of Nursing | Nurse Tutors | 4 |
ii. ST.GASPAR School of Nursing | Nurse Tutors | 5 |
KANDA YA MASHARIKI (EASTERN ZONE) | ||
i. KIBAHA Clinical Officers Training Centre (COTC) | Medical Doctors Assistant Medical Officers (AMO) | 4 3 |
ii. KILOSA Clinical Officers Training Centre | Medical Doctors Asst Medical Officer (AMO) | 4 |
KANDA YA ZIWA ( LAKE ZONE ) | ||
i. Bugando Asst Medical Officers Training Institute (AMOTIC) | Medical Doctors Medical Specialist | 4 1 |
ii. KOLANDOTO School of Nursing | Nurse Tutors | 6 |
iii. MUSOMA Clinical Assistants Training Centre (CATC) | Medical Doctors Asst Medical Officers (AMO) | 2 3 |
iv. NDOLAGE School of Nursing | Nurse Tutors | 5 |
v. RUBYA School of Nursing | Nurse Tutors | 3 |
vi. SENGEREMA School of Nursing | Nurse Tutors | 6 |
KANDA YA KASKAZINI (NORTHERN ZONE) | ||
i. HAYDOM School of Nursing | Nurse Tutors | 4 |
ii. HURUMA School of Nursing | Nurse Tutors | 5 |
iii. KCMC Asst. Medical Officer Training Centre | Medical Doctors Specialists | 4 2 |
iv. KCMC School of Nursing | Nurse Tutors | 5 |
v. KIBOSHO School of Nursing | Nurse Tutors | 3 |
vi. MUHEZA School of Nursing | Nurse Tutors | 4 |
vii. TANGA Dental Therapist School | Dental Surgeons | 2 |
viii. TANGA Asst. Medical Officer Training Centre | Medical Doctors | 3 |
ix. TANGA School of Nursing | Nurse Tutors | 3 |
KANDA YA KUSINI (SOUTHERN ZONE) | ||
i. LINDI Clinical Officer Training Centre | Medical Doctors | 6 |
ii. MASASI Clinical Asst Training Centre | Medical Doctors | 1 |
iii. MASASI Clinical Asst Training Centre | Asst Medical Officers | 2 |
iv. MTWARA Clinical Asst Training Centre | Medical Doctors | 6 |
v. NDANDA School of Nursing | Nurse Tutors | 2 |
vi. NEWALA School of Nursing | Nurse Tutors | 3 |
NYANDA ZA JUU KUSINI (SOUTHERN HIGHLANDS ) | ||
i. ILEMBULA School of Nursing | Nurse Tutors | 2 |
ii. MAFINGA Clinical Officer Training Centre | Medical Doctors | 4 |
iii. PERAMIHO School of Nursing | Nurse Tutors | 6 |
NYANDA ZA JUU KUSINI MAGHARIBI (SOUTHERN WESTERN HIGHLAND) | ||
i. Mbeya Asst Medical Officer Training Centre | Medical Doctors | 3 |
ii. SONGEA Clinical Asst. Training Centre | Medical Doctor | 1 |
iii. SUMBAWANGA Clinical Asst. Training Centre | Medical Doctor Asst. Medical Officers | 2 |
KANDA YA MAGHARIBI (WESTERN ZONE) | ||
i. KABANGA School of Nursing | Nurse Tutors | 3 |
ii. KIGOMA Clinical Asst Training Centre | Medical Doctors | 2 |
iii. NKINGA School of Nursing | Nurse Tutors | 4 |
Jumla | 137 |
Izingatiwe kwamba:
- Ajira ndani ya mradi huu itatolewa kwa mkataba wa miaka miwili. Kwa wale wote watakaofanikiwa kumaliza vipindi vyao vya mikataba, wataajiriwa katika utumishi wa umma.
- Watumishi waliopo katika ajira ya utumishi wa umma au katika Taasisi/Vyuo vya mashirika ya dini (FBOs) hawaruhusiwi kuomba nafasi hizi.
- Mishahara itatolewa kwa mujibu wa Waraka wa Maendeleo ya Utumishi Na. 1 wa mwaka 2009 kulingana na sifa na ujuzi wa mtumishi husika pamoja na maslahi mengineyo yaliyobainishwa katika mradi.
- Kwa taratibu za Serikali, wataalamu wenye umri chini ya miaka 45 wanashauriwa kuomba zaidi, na watakuwa na fursa kubwa ya ajira yao kuingia serikalini kwa masharti ya kudumu na pensheni. Kwa wataalamu wenye umri zaidi ya miaka 45 au waliostaafu, maombi yao pia yatashughulikiwa na ajira ya serikali itakuwa kwa mkataba.
- Barua ya maombi ya kazi, ikipendekeza Halmashauri 3 mwombaji anayopendelea kupangwa kazi, na pia aonyesha ridhaa ya kujiunga na utumishi wa umma, baada ya mkataba wa miaka miwili kumalizika.
- Nakala ya cheti cha Taaluma na cheti cha kidato cha 4 pamoja na cha 6 (iwapo anacho), na viwe vimethibitishwa na Hakimu au Wakili.
- Picha mbili (2) – saizi ya Pasipoti na maelezo binafsi (CV), ikionyesha umri, anuani kamili na namba ya simu ya kiganjani, pamoja na anuani/ namba ya kiganjani ya wadhamini wako.
Mwisho wa kupokea maombi haya ni tarehe 15 Juni 2011
Maombi yote yatumwe kwa:
Katibu Mkuu, Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, S.L.P. 9083, DAR ES SALAAM.
Tangazo hili linapatikana pia katika tovuti ya http://www.moh.go.tz