Wednesday, August 19, 2015

JOKATE: WAZAZI WASIINGILIE MAPENZI YA WATOTO....SOMA HAPA ALICHOKISEMA



JOKATE: WAZAZI WASIINGILIE MAPENZI YA WATOTO....SOMA HAPA ALICHOKISEMA
Staa wa Bongo, Jokate Mwegelo 'Kidoti'.
SIKU chache baada ya gazeti dada ya hili la Ijumaa Wikienda kuripoti juu ya wazazi wa Jokate Urban Mwegelo 'Kidoti' kumkataa Ali Kiba kama mchumba wake, binti huyo ameibuka na kuwataka wazazi kote nchini kuacha kuwaingilia watoto wao katika masuala ya kimapenzi, akidai jambo hilo ni vema wakiachiwa wenyewe.

Akizungumza na gazeti hili, Jokate alisema ni vyema kama wazazi wakawaacha watoto wao waoe au kuolewa na watu wawapendao, kwani vinginevyo ni kuwaingilia maisha na uhuru wao binafsi, jambo ambalo si jema.



"Unajua nimelala, madai ya Ally (Kiba), sitaki kuyazungumza sana, unajua mimi ni binti mtu mzima, ninao uhuru wa kumchagua nimpendaye kwa ajili ya maisha yangu, ifike mahali wazazi wawape uhuru watoto wa kufanya mambo yao, awamu hii siko tayari kuona naumizwa tena na familia juu ya uhusiano wangu," alisema binti huyo kwa njia ya simu juzi