Friday, April 10, 2015

Mgomo wa Mabasi: Tax Zapanda Bei Musoma....Kutoka Musoma Kwenda Mwanza ni Laki 4..Bus strike



Mgomo wa Mabasi: Tax Zapanda Bei Musoma....Kutoka Musoma Kwenda Mwanza ni Laki 4..Bus strike

Abiria zaidi 1000 waliokuwa wakisafari kutoka Musoma kwenda Dar es salaam kupitia mikoa ya Mwanza na Shinyanga na wale wa kwenda mpakani mwa Tanzania na Kenya Sirari pamoja na wa ndani ya mkoa wa Mara wameshindwa kusafari baada ya madareva kuitisha mgomo.

Baadhi ya madereva ambao wamekutwa katika kituo kikuu cha mabasi ya Bweri mjini Musoma,wamesema kuwa mgomo huo umeitishwa kwa ajili ya kupinga agizo la serikali la kukataa kusajili upya leseni zao hadi baada ya kwenda kusoma katika vyuo vinavyotambulika serikalini.

Kwa upande wao baadhi ya abiria wamesikitishwa na mgomo huo wa madereva ambao umesababisha hata wagonjwa kushindwa kusafiri hivyo wameitaka serikali kuchukua hatua za kumaliza migomo hiyo ambayo wamesema imekuwa kero kubwa kwa wananchi.

Abiria hao wameshuhudiwa wakiwa wamesimama kwa makundi katika kituo hicho kikuu cha mabasi huku magari makubwa ya abiria yakishindwa kuingia kabisa kituoni hapo hatua ambayo imesabisha baadhi ya abiria kulazimika kukodisha magari madogo aina ya taxi kwenda jijini Mwanza kwa gharama ya shilingi laki nne kutoka laki mbili za kawaida.
------------------------------------
More passengers in 1000 who travels from Musoma to Dar es Salaam via Mwanza and Shinyanga regions and those going to the border of Tanzania and Kenya Sirari with internal Mara failed to convene madareva trip after the strike.

Some drivers who are found in the center of Bweri buses in Musoma, have said that the strike has been called for opposing the government kept refusing to register their licenses renewed until after college to study at recognized government.

For their part some of the passengers have been disappointed with the strike of drivers that has led to patients failing to travel so have urged the government to take steps to end the strikes that which they say has been a great nuisance to the public.

Passengers they have witnessed standing in groups at the center's main bus with major automobile passenger failing to sign quite center stage which led to some passengers having to hire small cars form a taxi to go in Mwanza at the expense of hundred thousand shillings four from two lac common .