Thursday, February 26, 2015

HUKUMU YA KIFO KWA WAGENI-INDONESIA




HUKUMU YA KIFO KWA WAGENI-INDONESIA Indonesia's President Joko Widodo          listens as Malaysian Prime Minister Najib Razak (unseen) speaks          during a joint press conference at the prime minister's office          in Putrajaya, outside Kuala Lumpur on February 6, 2015. 

Rais wa Indonesia Joko Widodo alisema mataifa ya kigeni yasiingilie haki ya nchi yake kutumia hukumu ya kifo.

Anapata shinikizo kutoka viongozi wa  Australia, Brazil na France, ambao raia wake ni miongoni mwa watu 11 wanaokabililiwa na hukumu ya kifo kwa makosa ya kufanya biashara ya dawa za kulevya.




Bw Widodo alisema kuwa hukumu hiyo kwa kufyatuliwa risasi itatekelezwa.

Awali, mahakama ya Jakarta ilitupilia mbali rufaa ya raia wawili wa Australia waliyoombewa na rais wao ya kupunguziwa hukumu.

Indonesia ni moja ya nchi yenye adhabu kali mno duniani dhidi ya biashara ya dawa za kulevya. 

Ilifufua hukumu ya kifo mwaka 2013 baada ya kusimamishwa kwa miaka minne na kiongozi mpya Bw Widodo anachukua hatua kali zaidi kuhusu suala hilo.

Mwezi Januari, wauzaji sita wa dawa za kulevya –  watano wakiwa raia wa kigeni – waliuawa.

Duru ya pili ya kutekelezwa hukumu hiyo inayohusu watu 11 inatarajiwa kufanyika katika siku za hivi karibuni.