Wednesday, January 07, 2015

MCHEPUKO UNAPOGONGA MWAMBA


MCHEPUKO UNAPOGONGA MWAMBA
Mara baada ya kutokea kwa tatizo la gari kubwa kuziba njia katika eneo la Kiwangwa Wilayani Bagamoyo,magari mengi yalilazimika kutafuta njia mbadala ya kukwawezesha kuendeela na safari zao,lakini bahati mbaya huku nako kukatokea lingine na lori la mchanga kukwama kwenye udongo na kusababisha adha nyingine kwa wasafiri waliokuwa wakitumia njia hii.
Lori hilo likiwa limekwama kwenye dongo kutokana na uzito mkubwa liliokuwa nao,hali iliyopelekea adha nyingine kwa watumiaji wa njia hiyo.
Sehemu ya Abiria waliokuwa kwenye magari mbali mbali yaliyokwama katika eneo hilo walilazimika kutembea kwa miguu kuelekea barabara kubwa ili kuona kama watafanikiwa kupata usafiri.