Wednesday, January 07, 2015

HONGERA MWENYEKITI MPYA


HONGERA MWENYEKITI MPYA
Makamu Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa,Mh. Mboni Mhita (kushoto) akimpongeza Mwenyekiti Mpya wa Serikali ya Mtaa wa Masaki,Kinondoni Jijini Dar es Salaam,Ndg. Kimweri Mhita wakati wa hafla fupi ya kumpongeza mara baada ya kuapishwa kwake,Kimweri ni mmoja wa Wenyeviti wapya waliochagulia katika Uchaguzi uliofanyika hivi karibuni nchini kote. 
Mwenyekiti Mpya wa Serikali ya Mtaa wa Masaki,Kinondoni Jijini Dar es Salaam,Ndg. Kimweri Mhita (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Wazazi wake,Dkt. Mohamed Mhita (kushoto) na Mh. Zabein Mhita (Mbunge wa Jimbo la Kondoa Kaskazini) wakati wa hafla fupi ya kumpongeza mara baada ya kuapishwa kwake,Jijini Dar es Salaam jana.