Monday, December 29, 2014

TANZANIA FELLOWSHIP CHURCHES KUFANYA MKESHA MKUBWA WA KITAIFA KULIOMBEA TAIFA.


TANZANIA FELLOWSHIP CHURCHES KUFANYA MKESHA MKUBWA WA KITAIFA KULIOMBEA TAIFA.
                             Na Bakari  Issa,Dar  es Salaam.

Uongozi  wa  Tanzania Fellowship  Churches  unatarajia kufanya mkesha  mkubwa  kitaifa wa kuliombea  Taifa,Desemba 31 katika uwanja wa Taifa jijini  Dar es Salaam.

Mkesha huo una lengo la kuliweka Taifa mbele ya usalama wa Mungu pamoja na kupatikana amani  na utulivu kwa Taifa zima kwa ujumla.

Akithibitisha kuwepo kwa  mkesha huo   kitaifa,Mwenyekiti  wa mkesha  huo kitaifa,Mchungaji  Geodfrey  Mallasy  amesema mkesha huo una lengo  la kuliombea  Taifa  na kupatikana amani na utulivu.

"Mkesha huu una lengo la kuliweka Taifa  letu mbele ya usalama wa  Mungu na kuliombea Taifa letu  amani  na utulivu kutokana na bila amani hakuna kinachowezekana"alisema  Mallasy.

Aidha,Mallasy ameeleza kuwa mkesha huo  utahudhuliwa na mgeni rasmi ambaye ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt.Mohammed  Gharib Bilal badala ya Rais Jakaya Kikwete kuomba radhi kutokana na tatizo la kiafya.


Hata hivyo,uongozi  wa Tanzania Fellowship umeandaa usafiri kwa kampuni ya mabasi ya UDA kutoa huduma ya usafiri siku ya mkesha,pamoja na kutengeneza  timu moja ya waimbaji,kukusanya sadaka zikazosaidia kuandaa  mkesha mwingine utakaokuja