Wednesday, November 05, 2014

SHUKURANI TOKA FAMILIA YA MAREHEMU MZEE ANGULILE MWASUMBWE WA TUKUYU


SHUKURANI TOKA FAMILIA YA MAREHEMU MZEE ANGULILE MWASUMBWE WA TUKUYU
Kwa niaba ya familia ya mzee Angulile Mwasumbwe wa Kanyelele Tukuyu Mbeya, tunawashukuru ndugu, marafiki na jamaa zetu wote walioungana nasi kwa hali na mali katika msiba wa baba yetu uliotokea 23/09/2014. 
Mungu hatawapungukia wala kuwaacha.
 Tunamtukuza Bwana awezaye kutufanyia mambo ya ajabu kuliko vile tuwazavyo na tuombavyo (Efeso 3:20); tunamtukuza Mungu kwa kumtwaa Baba yetu katika uzee mwema - Marehemu ameishi miaka 100 kamili (1914 - 2014)
Mbarikiwe Mungu aliye Juu na jina la Bwana lihimidiwe!
 Michael Mwasumbwe Angulile
Marehemu Mzee Angulile Mwasumbwe enzi za uhai wake
Mdau Michael Angulile Mwasumbwe akiwa na babayake enzi alipokuwa hai
Michael na baba
Wakati wa mazishi huko kijijini Manyele, Tukuyu, Mbeya