Naibu Mwakilishi wa                Kudumu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Umoja wa                Mataifa Balozi Ramadhan Mwinyi akichangia majadiliano                kuhusu ajenda ya uthibiti wa silaha za nyukilia hapo siku                ya jumanne. Akizungumza msimamo wa Tanzania kuhusu silaha                hizo, Balozi Mwinyi amezitaka nchi zinazomiliki silaha                hizo kuonyesha utashi wa kisiasa wa kuzipunguza na                kuzidhibiti ili zisisambae kiholela lakini pia                waihakikishie dunia usalama wake. 
                Sehemu ya wajumbe wa                Kamati ya Kwanza ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa,                wakifuatilia majadiliano kuhusu upunguzaji wa silaha za                nyukilia ambapo wazungumzaji wengi pamoja na Tanzania                walisisitiza haja na umuhimu wa kuwa na maeneo huru yasiyo                na silaha za nyukilia kwa usalama wa dun dunia na wakatoa                wito kwa Shirika linalohusika na masuala ya Nguvu za                Nyukilia kuhakikisha kwamba kila nchi inakuwa na haki ya                kupata elimu na teknolojia inayohusiana na nguvu za                nyukilia bila ubaguzi au upendeleo.
         
