Shirika la Nyumba NHC leo                limesaini mkataba na Halmashauri ya Wilaya Mpya ya                Busokela iliyopo Mkoani Mbeya ya Ujeni wa Nyumba 5,000 za                garama nafuu.Utiaji saini makubaliano hayo umefanyika leo                mchana katika Hoteli ya New Dodoma mjini Dodoma na                kuhudhuriwa na Wabunge wanaotoka Mkoa wa Mbeya wakiongozwa                na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Asiye na Wizara Maalum.
         Mhe.Prof Marck                Mwandosya,Waziri, ambaye Wilaya hiyo Mpya iko katika Jimbo                lake la Rungwe MasharikiMawaziri mwingine aliyehudhuria                hafla hiyo ni Waziri wa Uchukuzi Mhe.Harrison Mwakyembe na                kushuhudiwa na Naibu Waziri,Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za                Mikoa na Serikali za Mitaa,(TAMISEMI) Mhe.Aggrey Mwanri. 
                Pichani wanaosaini kuanzia                kulia ni kaimu Mkurugenzi Mkuu wa NHC,Bwa.Felix                Maagi,Bw.Meckson Mwakipunga (Mwenyekiti wa Halmashauri ya                Wilaya Mpya ya Busokela iliyopo Mkoani Mbeya na Bw. Said                Mderu. 
                Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa                NHC,Bwa.Felix Maagi akibadilishana Mkataba na Mwekiti wa                Halmashauri ya Wilaya Mpya ya Busokela Bw.Meckson                Mwakipunga baada ya kutiliana saini Ujenzi wa nyumba 5,000                katika Wilaya Mpya ya Busokela iliyopo Mkoani Mbeya. 
                Mwenyekiti wa Halmashauri ya                Wilaya Mpya ya Busokela Bw.Meckson Mwakipunga akielezea                kuhusu Mradi mzima, baada ya kutiliana saini Ujenzi wa                nyumba 5,000 katika Wilaya Mpya ya Busokela iliyopo Mkoani                Mbeya . 
                Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais                Asiye na Wizara Maalum. Mhe.Prof Marck Mwandosya. Waziri                ambaye Wilaya hiyo Mpya iko katika Jimbo lake la Rungwe                Mashariki akitoa shukurani baada ya mkataba Ujeni wa                Nyumba 5,000 za garama nafuu kusainia. 
                Baadhi ya Wabunge wanaotoka                Mkoa wa Mbeya wakifuatilia utiaji saini wa Mkataba wa                Ujeni wa Nyumba 5,000 za garama nafuu katika Halmashauri                ya Wilaya Mpya ya Busokela iliyopo Mkoani Mbeya.Picha na                Deusdedit Moshi wa Michuzi Blog Kanda ya Kati 
        




 
