Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Blantyre nchini Malawi kwa ajili ya kushiriki mazishi ya aliyekuwa Balozi wa Malawi nchini Tanzania, Marehemu Flossie Gomile-Chidyaonga aliyefarikii dunia tarehe 09 mei, 2014 Jijini na Dar es Salaam na anatarajiwa kuzikwa tarehe 14 Mei, 2014. Mhe. Membe anamwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete kwenye mazishi hayo.  | Balozi wa Tanzania nchini Malawi, Mhe. Patrick Tsere akimweleza jambo Mhe. Membe wakati wa mapokezi. |  | Mhe. Membe akijaribu kumwelezea Rais wa Malawi, Mhe. Joyce Banda namna alivyozipokea taarifa za kifo cha Balozi Flossie. Kushoto kwa Mhe. Rais Banda ni mume wake Jaji Mkuu Mstaafu Banda na kulia kwa Mhe. Membe ni Waziri wa Mambo ya Nje wa Malawi, Mhe. Ephraim Chiume. | |