Thursday, November 15, 2012

Kumbukumbu




Askofu Stephen Mwakasyuka (1933-2008)

Leo tarehe 15/11/2012 imetimu miaka minne tangu tulipoondokewa na Baba yetu mpendwa Askofu Stepen Mwakasyuka. Wakati anaondoka tuliumia mno na wengine kujiona kuwa na hatia ya kushindwa kufanya kila lililowezekana kuokoa maisha yake.

Tukiwa bado katika kipindi cha uchungu mkubwa, wakaondoka waliokuwa wakitufariji wakiwemo akina John Samwel Mwakasungura, Tulinagwe Mbangula, Jimmy David Ngonya, Kyomba Mwaipopo, na hivi karibuni Jimmy Mwabwagilo, Ashery Mwasandube, Amon Mwakatobe na Spendi Mwalisatile. Katika hili tumejifunza na kuamini kuwa ni kweli hapa duniani sote tu wapitaji.

Sisi tuliobaki katika Familia akina Ezeline, Phoebe, Florence, Jossey, Tungibwaga, Mponjoli, Atuganile, Frida, Salome, Gwakisa, Christian na Lazaro, tunazidi kuliwazwa na kufarijiwa na Hazina tuliyonayo ya Ndugu, Jamaa, Marafiki na Wapendwa waliopo, tukiamini kwamba iko siku sote tutaja onana Paradiso.

Wafilipi 4:6