Friday, September 21, 2012

UKUAJI WA KASI WA MAENDELEO JIMBO LA KISESA MKOANI SIMIYU. JK ATUNUKIWA HATI KWA KUTEKELEZA AHADI, MPINA ASIMIKWA UCHIFU.


Mbunge wa Kisesa wilaya ya Meatu mkoani Simiyu (CCM), Luhaga Joelson Mpina, akionyesha hati ya Pongezi  na  Shukurani kwa Mheshimiwa Rais Jakaya Mrisho Kikwete, ikiwa ni kutambua mchango wake kwa maendeleo ya Jimbo la Kisesa na Kasi yake katika kuboresha huduma, kusukuma ukuaji wa uchumi  na kuwaletea maendeleo Watanzania, hati iliyotolewa na Jumuiya ya Wananchi wa Jimbo la Kisesa.


Hati ya Pongezi  na  Shukurani kwa Mheshimiwa Rais Jakaya Mrisho Kikwete, ikiwa ni kutambua mchango wake kwa maendeleo ya Jimbo la Kisesa na Kasi yake katika kuboresha huduma, kusukuma ukuaji wa uchumi  na kuwaletea maendeleo Watanzania.

Kikundi cha kwaya ya CCM kijiji cha Mwandoya Jimbo la Kisesa kikitumbuiza kusanyikoni.

Moja kati ya sababu zilizopelekea kwa wananchi wa Jimbo la kisesa kumtunuku Rais Kikwete Hati ya Kasi ya Maendeleo ni kitendo cha kutimiza ahadi ya kulipatia jimbo hilo umeme,  Uimarishwaji na uboreshwaji wa huduma za Elimu, Afya na Barabara pamoja na hivi karibuni Serikali kuahidi kutoa kiasi cha 6M/- kulipa fidia ya ng’ombe 22 wanaodaiwa kuuawa kwa kupigwa risasi na askari wa wanyamapori wa pori la akiba Maswa wilayani Meatu, mkoani Simiyu.
Inadaiwa ng,ombe hao walipigwa risasi na kuuawa Desemba 2009 baada ya kuingizwa kuchungia ndani ya hifadhi hiyo, kitendo ambacho ni kinyume na sheria zinazolinda hifadhi za wanyama pori.

Mtangazaji wa kituo cha televisheni cha Star Tv Abdalah Tilata (mwenye miwani kushoto) akipata flash na marafiki Jimboni Kisesa.

"Mheshi miwa Mbunge Shabaha ya mapokezi haya nikukupongeza mbunge wetu kwa jinsi unavyotetea hoja zetu Bungeni na kwamba katika kipindi chako cha uwakilishi tumeshuhudia mapinduzi ya maendeleo kuliko vipindi vyote vilivyopita...." kisha lisala ikaendelea ... "...Tunakupongeza kwa jinsi unavyotoa muda wako kwa masuala ya maendeleo jimboni kwetu"

Mbunge Luhaga Mpina akivishwa vazi maalum la jadi ya kabila la Wasukuma kwa ajili ya kusimikwa rasmi kuwa Chifu.

Kiongozi wa jadi kabila la Wasukuma akimsimika mbunge Luhaga Mpina kwenye mkutano wa kujadili masuala ya maendeleo jimboni Kisesa mkoa mpya wa Simiyu huku wakishuhudiwa na wananchi wa kijiji cha Mwandoya waliofurika kwa wingi.

Shughuli za usimikwaji zikiendelea....

Wananchi  wa kijiji cha Mwandoya wakimsikiliza mgombea wao wakati alipopewa nafasi kuhutubia.

"Kamwe tusichoke kuyatafuta maendeleo.. na juhudi zimefanikiwa kutufikisha hapa kutokana na umoja wetu na dhamira yetu tuliyojiwekea... Hivyo basi tusichoke kushikamana na kuwajibishana pale tunapokosea" Alisema Mhe. Mpina kwenye sehemu ya hotuba yake.

Mhe. Mpina naye ni mkali katika kuimba.......

SABABU ZA MPINA KUKUBALIKA JIMBONI KWAKE:
Jimbo la Kisesa lilikuwa ni miongoni mwa majimbo yasiyo na miundombinu ya uhakika kuweza kupitika katika kipindi chote cha mwaka iwe masika au kiangazi (G. Sengo blog imekuwa shuhuda) lakini kupitia uwakilishi awamu moja na robo sasa wa Mh. Mpina barabara zinapitika kwa uhakika mwaka mzima hali inayosaidia ukuaji wa kasi wa uchumi jimboni humo.
Sehemu ya hotuba.....