Monday, March 07, 2016

NIPE FAGIO YAUNGANA NA WAENDESHA BAJAJI KATIKA ZOEZI LA USAFI WA MTO MLALAKUWA JIJINI DAR


NIPE FAGIO YAUNGANA NA WAENDESHA BAJAJI KATIKA ZOEZI LA USAFI WA MTO MLALAKUWA JIJINI DAR
Waendesha Bajaj kituo cha Survey kilichopo Mlalakua Dar es Salaam wakifanya usafi na baadhi ya wajumbe wa Taasisi ya Nipe Fagio kwenye eneo la pembezoni mwa mto Mlalakua baada ya taasisi hiyo kuwakabidhi vifaa mbalimbali vya usafi na programu ya usafi wa mto huo.
 Tania Hamilton, Mkurugenzi wa Taasisi ya Nipe Fagio inayoshughulikia uhifadhi mazingira akizungumza na Mwenyekiti wa Waendesha Bajaj wa Kituo Cha Survey, Aloyce Cassian wakati wa kufanya usafi katika eneo la Mto Mlalakuwa Dar es Salaam jana baada ya taasisi hiyo kuwakabidhi vifaa mbalimbali vya usafi na programu ya usafi wa mto huo.
Tania Hamilton, Mkurugenzi wa Taasisi ya Nipe Fagio akizungumza na waendesha Bajaj wakati wa kufanya usafi katika eneo la Mwenge Dar es Salaam jana baada ya taasisi hiyo kuwakabidhi vifaa mbalimbali vya usafi na programu ya usafi wa mto huo.