Thursday, August 13, 2015

44 WATEKETEA KWA MOTO HADI KUFA TIANJIN CHINA



44 WATEKETEA KWA MOTO HADI KUFA TIANJIN CHINA
Eneo la viwanda vya Tianjin
Vyombo vya habari China vinasema watu arobaini wamefariki kutokana na milipuko mikubwa katika kiwanda.


Kituo cha reli kilichoharibiwa
Manusura wa mkasa huo
Moshi mweusi bado umetanda kutoka ghala hilo lililopo katika mji wa bandari wa Tianjin ambako milipuko ilitokea jana usiku.
Mlipuko huo uliharibu kabisa eneo la viwanda
Mabweni ya wahamiaji yaliporomoka kutokana na milipuko hiyo.
Magari aina ya Volkswagen yaliyoteketea
Video zilizowekwa katika mitandao ya kijamii zinaonyesha moto mkubwa na wingu kubwa la moshi lililotanda angani.
Magari aina ya Volkswagen yaliyoteketea
44 waliteketea hadi kufa Tianjin China
Eneo hilo lenye viwanda liliharibiwa lote
Mlipuko huo mkubwa katika mji wa China Tianjin-ambao ni mji wa Bandari kuu na sehemu ya viwanda katika eneo la kusini kaskazini mwa mji mkuu Beijing unadaiwa kuwajeruhi mamia ya watu ingawa kufikia sasa idadi kamili haijulikani.
Moto uliofuatia mlipuko
Shirika la habari la nchi hiyo, Xinhua limesema mlipuko huo ulisababishwa na kemikali zilizokuwa zimehifadhiwa katika bohari moja katika bandari hiyo.
BBC.