Sunday, April 05, 2015

WANANCHI KENYA WAOMBOLEZA SHAMBULIZI LA GARISSA



WANANCHI KENYA WAOMBOLEZA SHAMBULIZI LA GARISSA
Shambulizi hilo la siku ya Alhamisi liliwaacha takriban watu 150 wakiwa wameuawa.

Shirika la msalaba mwekundi nchini Kenya linasema kuwa hadi sasa maiti 54 zimetambuliwa katika chumba kimoja cha kuhifadhi maiti kwenye mji mkuu wa Kenya Nairobi.


Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta amesema kuwa idara za usalama zinahitaji kuongeza jitihada za kupambana na wanamgambo wa Al shabaab.

Chuo cha kutoa mafunzo ya kiislamu kinacheshimiwa zaidi nchini Misri, Al-Azhar kimelaani kile ilichokitaja kuwa shambulizi la kigaidi dhidi ya wanafunzi wasio na hatia.