Waziri wa Fedha Mhe. Saada Salum              Mkuya akimsikiliza kwa makini Mwakilishi Mkazi wa Benki ya              Dunia Tanzania, Rwanda, Uganda na Burundi Bw. Philippe              Dongier walipokutana katika mikutano hii ya kipupwe              inayoendelea hapa Mjini Washington DC.Wengine ni ujumbe              kutoka Tanzania pamoja na timu ya wataalam kutoka Benki ya              Dunia.
        Waziri wa Fedha Mhe. Saada Salum              akifuatilia kwa makini maswalialiyokuwa akiulizwa na              Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Dunia Tanzania, Rwanda, Uganda              na Burundi Bw. Philippe Dongier hayupo kwenye picha. Kulia              ni katibu Mkuu Wizara ya Fedha Zanzibar Bw.
                Ujumbe wa Mkutano huo kutoka pande              zote mbili yaani Tanzania na Benki ya Dunia, wakimsikiliza              kwa makini Mchumi mwandamizi kutoka Benki ya Dunia.
                Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na              Mlipaji Mkuu wa Serikali Dr. Servacius Likwelile              akijadiliana jambo na Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Dunia              Tanzania, Rwanda, Uganda na Burundi Bw. Philippe Dongier              kabla ya kikao kuanza rasmi.
                Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na              Mlipaji Mkuu wa Serikali Dr. Servacius Likwelile akiandika              kwa makini hoja na mapendekezo yaliyokuwa yakitolewa na              Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Dunia Tanzania, Rwanda, Uganda              na Burundi Bw. Philippe Dongier.
                Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na              Mlipaji Mkuu wa Serikali Dr. Servacius Likwelile akijibu na              kueleza kwa umakini hoja na mapendekezo yaliyokuwa              yametolewa na Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Dunia Tanzania,              Rwanda, Uganda na Burundi Bw. Philippe Dongier.
        …………………………………………………
        Wakati Tanzania ikiendelea              kupambana na umaskini , Benki ya Dunia imesema kuwa,"              tumefurahishwa sana na mwenendo mzuri wa usimamizi wa fedha              na bajeti". Hayo yalisemwa na Mwakilishi Mkazi wa Benki ya              Dunia Tanzania, Rwanda, Uganda na Burundi Bw. Philippe              Dongier katika mkutano ambao waziri wa Fedha Mhe. Saada              Mkuya Salum alikuwepo.
        Mambo mbalimbali yalizungumziwa              katika mkutano huo ambapo suala la upatikanaji wa fedha              kusaidia bajeti ya serikali lilipewakipaumbele.Maboresho              katika Sekta ya umeme nalo jambo mojawapo liliopewa uzito              kwani Nchi wahisani wamepata moyo wakuachia misaada baada ya              kuona Serikali imeweza kulishughulikia suala zima la IPTL.
        " Nchi wahisani wamekubali              kuendelea kutoa misaada kwa asilimia mia, hii ni kwa sababu              tu! serikali yenu imekubali kuchukua hatua dhidi ya tatizo              la IPTL", alisema Philippe.
        Akizungumza na waandishi wa habari              Mhe. Mkuya alisema kuwa, suala la kuboresha Pension nalo              lilizungumziwa na chombo hiki kitasaidia serikali katika              kuboresha malipo ya uzeeni (pension) na kuwezesha mashirika              ya "pension" ili yaweze kuwa na uwezo wa kusaidia wastaafu.              Aidha tumekubaliana kuwa watatusaidia katika suala zima la              kuboresha uwazi serikalini na mazingira ya biasha              Tanzania.Aliongeza Mkuya.
        Jambo lingine lililochukua uzito              katika majadiliano hayo ni suala la kufanya ukaguzi              Bandarini. Hili limejitokeza baada ya kubainika kuwa kuna              baadhi ya wafanya biashara sio waaminifu hivyo benki ya              Dunia imeitaka Serikali kuangalia upya maamuzi ya mwanzo ya              serikali yakuto kagua mizigo, na kusema kuwa wanasubiri              majibu juu ya kubadilisha utaratibu wa mwanzo. Tanzania              imekubali kukaa kwa pamoja Wizara na Fedha na TRA ili              kurudisha majibu na mkakati ambao kama serikali watakuwa              wamekubaliana.
        "Kumekuwa na madai mengi ambayo              yanadaiwa na makandarasi na wafanyabiashara wadogo,              tutajitahidi kuyalipa iliyaishe lakini kwa wale wenye              nyaraka halali, tunaenda kupiga marufuku kwa Afisa masuuli              wote kuwa kuanzia sasa hakuna kufanya malipo yoyote kama              hakuna fedha kwa ajili ya shughuli hiyo".Alisema Mkuya.
        " Hii itasaidia kupunguza madeni.              Ninasema haya kwani ndicho kitu tulichokubaliana kwenye              mkutano huu". Alisistiza Mkuya.
        Mikutano hiyo bado inaendelea hapa              mjini Washington DC. Hali ya hewa ni baridi kiasi.
        Imetolewa na Msemaji :Wizara ya fedha
Ingiahedi C.Mduma
Washington DC
16/04/2015
        Ingiahedi C.Mduma
Washington DC
16/04/2015