Wednesday, January 14, 2015

Mwenyekiti wa CCM Kata ya Miono,Saleh Mpwimbwi afariki Dunia leo


Mwenyekiti wa CCM Kata ya Miono,Saleh Mpwimbwi afariki Dunia leo
Mwenyekiti wa CCM Kata ya Miono,Ndg. Saleh Ramadhan Mpwimbwi (pichani) amefariki Dunia asubuhi ya leo kwa ajali ya Gari alilokuwa akiendesha mwenyewe, maeneo ya katikati ya Kijiji cha Hondogo na Miono.

Chanzo cha ajali hiyo,kinaelezwa kuwa ni kupasuka kwa tairi ya nyuma wakati akiwa kwenye mwendo na kushindwa kuliongoza gari hilo na kupelekea kupinduka.

Mwili wa Marehemu umepelewa kuhifadhiwa kwenye Hospitali ya Wilaya ya Bagamoyo.

Taratibu zote za msiba huo,zinafanyika Nyumbani kwake Miono,Wilaya ya Bagamoyo Mkoani Pwani.

Tunamuombea kwa Mungu aiweke Roho yake mahala pema peponi

-Amin