Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Yusuf Mwenda amekabidhi msaada wa vyakula wenye thamani ya shilingi milioni 2.5 kwa vituo vitatu vya kulelea watoto yatima vilivyopo kwenye Manispaa yake, Dar es Salaam ambavyo ni Missionary of Charity cha Mburahati, Almadina Children Home na Mwandaliwa Orphanage Centre cha Mbweni na kuwataka watu wenye uwezo kujitokeza kuvisaidia vituo hivyo ikiwemo kuasili watoto wanaolelewa kwenye kituo cha Missionary of Charity.
Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Yusuf Mwenda akisalimiana na watoto wanaolelewa kwenye kituo cha Missionary of Charity kabla ya kukabidhi msaada wa vyakula kwa kituo hicho katika hafla iliyofanyika kwenye Manispaa yake, Dar es Salaam.
Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Yusuf Mwenda akikabidhi msaada wa vyakula kwa mtoto Anitha Consantino wa kituo cha Missionary of Charity kwa niaba ya watoto wenzake wakati wa hafla iliyofanyika kwenye Manispaa yake, Dar es Salaam.
Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Yusuf Mwenda akikabidhi sehemu ya msaada wa vyakula na vitu mbalimbali kwa Mlezi wa Kituo cha kulelea watoto yatima cha Almadina Children Home, Kurthum Yusuf kwa niaba ya watoto wanaolelewa kwenye kituo hicho wakati wa hafla iliyofanyika kwenye Manispaa hiyo, Dar es Salaam.
Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Yusuf Mwenda akikabidhi sehemu ya msaada wa vyakula na vitu mbalimbali kwa mtoto Mwajabu Juma wa kituo cha kulelea watoto yatima cha Mwandaliwa Orphanae Centre kwa niaba ya watoto wenzake wakati wa hafla iliyofanyika kwenye Manispaa hiyo, Dar es Salaam.