Na Chalila Kibuda,Globu                ya Jamii
        Askofu Msaidizi wa Jimbo                kuu la Katoliki ,Dar es Salaam Eusebius Nzigilwa amesema                katika kuadhimisha sikukuu ya Krismas  watu wafuate njia                ya mungu na sio njia ya Ibilisi ambayo inafundisha maovu.
        Akizungumza leo baada ya                Ibada ya Sikukuu ya Krismas ,Nzigilwa alisema watu wenye                uwezo lazima wasaidie wasio na uwezo kwani Yesu alizaliwa                katika pango la Bethelehem lakini watu wenye uwezo                walimuacha kutokana na kuwa katika njia ya ibilisi.
        Nzigilwa alisema suala                la kuingiziwa fedha katika akaunti yake ambazo zilitoka                katika akaunti ya Tegeta Escrow hawezi kulizungumzia kwa                 sasa lakini siku zijazo atazungumzia suala hilo.
        Naye Askofu Mkuu wa                Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania  (KKKT),Dk. Alex                Malasusa alisema kuwa watu lazima wawe na hofu ya mungu                mambo yanayotokea sasa ya ufisadi yanaiweka nchi sehemu                mbaya.
        Malasusa aliyasema hayo                katika Ibada ya Krismas iliyofanyika katika Kanisa la                Azania Front ,alisema nchi ipo katika mambo ambayo                hayampendezi Mungu hivyo ni lazima tutoke huko ili                wananchi waandokane na kusikia ufisadi kwani sio maendeleo                ambayo yanatakiwa kwa sasa.
        Mkuu wa Kanisa Kuu la                 St.Albano ,Aidano Mbulinyingi alisema  jamii imeingia                kufanya vitendo viovu kutokana na kuacha maandiko ya mungu                hivyo tunahitaji kujenga msingi upya katika kutokomeza                vitendo hivyo ambapo mungu hapendezi navyo.
                 Askofu Msaidizi wa                Jimbo kuu la Katoliki ,Dar es Salaam Eusebius Nzigilwa                akiongoza ibada ya Krismas katika Kanisa la Mt.                Joseph,jijini Dar es salaam leo.
                "Shkamoo....." Askofu                Msaidizi wa Jimbo kuu la Katoliki ,Dar es Salaam Eusebius                Nzigilwa akipokea salam kutoka kwa mtoto,mara baada ya                Ibada ya Krismas katika Kanisa la Mt. Joseph,jijini Dar es                salaam leo.
         Askofu Mkuu wa Kanisa                  la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT),Dk. Alex                  Malasusa akiwatakia heri ya Krismas sehemu ya Waumini wa                  Kanisa la KKKT Azania Front,jijini Dar es Salaam leo.
          

