Tuesday, November 18, 2014

WANANCHI WA MTWARA WAHIMIZWA KUJIUNGA NA CHUO KIKUU HURIA TANZANIA



WANANCHI WA MTWARA WAHIMIZWA KUJIUNGA NA CHUO KIKUU HURIA TANZANIA
WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Hawa GHASIA akiwahutubia Viongozi wa mkoa wa Mtwara pamoja na wananchi wa mkoa wa Mtwara walio shiriki katika uzinduzi wa majengo ya tawi la Chuo kikuu huria Tanzania kushoto kwa waziri ni Makamu wa chuo kikuu huria Tanzania Profesa Tolly Mbwete kulia ni Mkuu wa mkoa wa Mtwara Halima Dendego Waziri Hawa Ghasia alimuakilisha Waziri Mkuu Mizengo Pinda katika uzinduzi wa majengo ya tawi la chuo kikuu huria Mtwara.
Makamu mkuu wa Chuo kikuu huria Tanzania Profesa Tolly Mbwete aliye vaa koti akimuonyesha WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Hawa GHASIA Vifaa vya kisasa kwa ajili ya kufundisha kwakutumia Intarnet katikati ni Mhadhiri wa taluma ya sayansi ya mtandao Dr Edephonce Ngemera Waziri Hawa Ghasia alikuwa akimuakilisha Waziri Mkuu Mizengo Pinda katika uzinduzi wa majengo ya tawi la chuo kikuu huria mkoani Mtwara.
WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Hawa GHASIA akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wengine wa Serikali pamoja na viongozi wa chuo kikuu huria mkoani Mtwara.Picha na Chris Mfinanga