Afisa biashara wa NMB Tawi                    la Mbalizi Road, Alex Masawe alisema msaada waliotuo                    ni kutokana na wafanyakazi wa Benki hiyo kuguswa na                    maombi ya mmiliki wa Kituo hicho akiomba msaada wa                    vifaa vya shule kwa watoto wawili wanaoenda vyuo vya                    ualimu.
                  
                  
                  Alivitaja vitu                    vilivyopelekwa kuwa ni pamoja na Matranka mawili,                    makufuri mawili, Mchele debe tatu, mashuka 4, sabuni                    katoni 4, mafuta ya kula lita 20,sabuni ya unga kilo                    20,nguo za ndani dazani 2, free style moja, mafuta ya                    kupaka dazani 2,miswaki dazani 5 na dawa za mswaki                    dazani 4.
                  
                  
                  Vingine ni vitambaa kwa                    ajili ya sare za chuo vya rangi nyeusi mita 6, mashati                    mawili, sabuni za kuogea dazani mbili, makaratasi aina                    ya manira 10, blanketi 4,unga wa sembe kilo 20,                    mahindi debe tatu, nyanya sado moja na vitunguu sado                    moja.
                  
                  
                  Masawe alisema hivyo vitu                    baadhi yake vitasaidia kituo na vingine ni kwa ajili                    ya wanafunzi waokwenda kusoma ambao sambamba na vitu                    hivyo pia walikabidhiwa fedha taslimu shilingi Laki                    moja na kufanya jumla ya vitu vilivyotolewa kuwa na                    thamani ya shilingi milioni 1.1.
                  
                  
                  bidii                  Kwa upande wake Mmiliki wa                    Kituo hicho, Annah 
                  Kasire mbali na kuipongeza                    benki ya NMB kwa msaada huo alisema vitu hivyo                    vitaleta chachu kwa wanafunzi kuongeza katika masomo                    yao.
                  
                  
                  Aliwataja wanafunzi wanoenda                    kusoma kuwa ni Magreth Mwasile na Tumain Mwampamba                    ambao wote kwa pamoja wanatarajia kwenda kusoma Chuo                    cha Ualimu kilichopo Nyororo mkoani Iringa na kuongeza                    kuwa hadi sasa kituo kinalea watoto 120.
                  
                  
                  Mwisho.
                  Na Mbeya yetu