Friday, October 31, 2014

TUTASHIRIKIANA NA WAPENDA AMANI KUISAIDIA DRC KUWA NA AMANI - TANZANIA



TUTASHIRIKIANA NA WAPENDA AMANI KUISAIDIA DRC KUWA NA AMANI - TANZANIA
Naibu Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Balozi Ramadhan Mwinyi akizungumza wakati wa Mkutano wa Kamati ya Nne ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa iliyokuwa ikijadili ajenda kuhusu tathmini ya jumla ya Operesheni za Ulinzi wa Amani za Umoja wa Mataifa. Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni kati ya nchi zinazochangia wanajeshi wake katika operesheni hizo za ulinzi wa amani.
Sehumu ya wajumbe wa Kamati ya Nne ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, wakifuatilia majadiliano ya ajenda kuhusu Operesheni za Ulinzi wa Amani za Umoja wa Mataifa.