Tuesday, September 30, 2014

TBL YAPATA TUZO YA HESHIMA WIKI YA NENDA KWA USALAMA




TBL YAPATA TUZO YA HESHIMA WIKI YA NENDA KWA USALAMA
 Mkuu wa Mkoa wa Manyara,Mbwilo, akimkabidhi Cheti cha kutambua chango mkubwa uliofanywa na Kampuni ya Bia nchini (TBL) ambayo iliendesha zoezi la upimaji afya kwa madareva, Meneja wa Kiwanda cha Bia Arusha Moshi  Sarvatory Rweyemamundiye aliyepokea kwa niaba ya uongozi wa Kampuni hiyo wakati wa kufunga Wiki ya Nenda kwa Usalama barabarani iliyofanyika kitaifa mkoani Arusha.
 Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani Marrison Mwakyoma akipima macho yake kama sehemu ya kuhamasisha upimaji wa fya kwa madereva wa mabasi na magari ya mizigo wakati wa wiki ya nenda kwa usalama barabarani zoezi hilo lilifanyika eneo la Makuyuni wilayani Monduli mkoani Arusha
Mkuu wa wilaya ya Monduli Jowika Kasunga akisisitia jambo wakati alipokuwa akipewa maelekezo ya namna wataalamu wanavyochukua vipimo vya afya kutoka kwa madereva wa mabasi na magari ya mizingo wakati wa zoezi la upimaji wa afya lililofanyika Makuyuni wilayani humo ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Wiki ya Nenda kwa Usalama barabarani