Tuesday, September 30, 2014

TANGAZO LA KIFO NA MAZISHI YA DR. HABIBA MUZA RAJABU



TANGAZO LA KIFO NA MAZISHI YA DR. HABIBA MUZA RAJABU
Marehemu Dr. Habiba Muza Rajabu wakati wa uhai wake.

Familia ya Marehemu Mzee Iddi Rajabu Mtoro wa Utemini, Singida inasikitika kutangaza kifo cha Dr. Habiba Muza Rajabu kilichotokea siku ya Jumamosi tarehe 27 Septemba 2014 hapa katika mji wa Trondheim, Norway.

Msiba uko Utemini, Singida na hapa Trondheim, Norway.

Dr. Habiba Muza Rajabu alishawahi kuwa Mhadhiri (Lecturer) katika Idara ya Chemistry, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Dr. Habiba Muza Rajabu atazikwa hapa katika mji wa Trondheim, Norway siku ya Jumatano, 1 Octoba 2014 majira ya saa 7 mchana katika eneo la Svanholm Hallen at Moholt. Kumuaga kuanzia saa 7 mchana hadi saa 7:45. Baada ya hapo maziko ya Kiislam yatafanyika hapo hapo.

INALILAHI WAINA ILAHII RAJUUN (HAKIKA SISI SOTE NI WA MWENYEZI MUNGU NA KWAKE TUTAREJEA)

Imetangazwa na: Rajabu Iddi Rajabu,