Tuesday, September 02, 2014

Tanzania Kuongoza Nchi za Afrika katika maboresho ya utoaji wa haki za watuhumiwa na mahabusu



Tanzania Kuongoza Nchi za Afrika katika maboresho ya utoaji wa haki za watuhumiwa na mahabusu
Mkurugenzi wa Idara ya Huduma za Kisheria kutoka Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Bw. Nabor Assey akiongea na waandishi wa Habari (Hawapo pichani) kuhusu utekelezaji wa Miongozo ya Luanda inayohusu ukamataji na ushikiliaji wa watuhumiwa kabla ya kufunguliwa mashtaka itakayosaidia kupunguza mzigo kwa seriikali katika uendeshaji wa mahabusu na magereza yenye msongamano mwingi wa watuhumiwa na wafungwa, wakati wa Mkutano leo Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Bi. Zamaradi Kawawa.
Afisa Mawasiliano Mwandamizi kutoka Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Bw. Germanus akiongea na waandishi habari (Hawapo pichani) wakati wa Mkutano leo Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Kaimu Mkurugenzi Idara ya Elimu kwa Umma na Mafunzo wa Tume hiyo Bw. Alexander Hassan.(Picha na Hassan Silayo-MAELEZO )