Saturday, September 20, 2014

MHE. BALOZI PHILIP MARMO AWEKA SAINI MKATABA WA MKOPO KUTOKA MFUKO WA MAENDELEO YA KIMATAIFA




MHE. BALOZI PHILIP MARMO AWEKA SAINI MKATABA WA MKOPO KUTOKA MFUKO WA MAENDELEO YA KIMATAIFA
Mhe. Balozi Philip S. Marmo wa Ubalozi wa Tanzania Ujerumani yuko Vienna, Austria tarehe 9 Septemba, 2014 kuweka saini Mkopo kwa mradi wa tatu wa kupunguza umasikini wa Dola za Marekani 16,350,000 na mradi wa kuendeleza Elimu wa Dola za Marekani 10,200.000. Miradi hiyo itatekelezwa na serikali ya Mapinduzi Zanzibar. Mheshimiwa Balozi Marmo anawakilisha pia Austria kutoka Ujerumani. Mkataba huo ulisainiwa katika ofisi za OFID, Vienna, Austria kati yake na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa OPEC kwa ajili ya Maendeleo ya Kimataifa, OPEC Fund for International Development(OFID) Bw. Suleiman J. Al-Herbish.
Balozi Philip S. Marmo akiweka saini Mkataba wa Mkopo kutoka Mfuko wa OPEC , OFID Ofisi ya OFID iliyopo Austria, Vienna tarehe 9 Septemba, 2014.
Balozi Marmo akipokea Nakala ya Mkataba wa Mkopo kutoka Mfuko wa OPEC kutoka kwa Bw. Suleiman J. Al-Herbish, Mkurugenzi Mkuu wa OFID-Mfuko wa Maendeleo wa OPEC , Austria, Vienna tarehe 9 Septemba.