Monday, September 15, 2014

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AKUTANA NA MBUNGE WA SHIRIKISHO LA UJERUMANI


MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AKUTANA NA MBUNGE WA SHIRIKISHO LA UJERUMANI
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal akizungumza na Mhe. Charles M. Huber (wa pili kushoto) ambaye ni Mbunge na Mjumbe wa Kamati ya Ushirikiano wa Uchumi na Maendeleo na Mambo ya Nje ya Bunge la Shirikisho la Ujerumani wakati alipofika Ofisini kwake Ikulu jijini Dar es Salaam kwa mazungumzo leo Septemba 15, 2014.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja na Mhe. Charles M. Huber (kulia kwa Makamu wa Rais), Stefan Reith Mwakilishi wa Konrad Adenauer Stiftung (KAS) kushoto, Naibu Balozi wa Ujeruman nchini John Reyels (wa pili kulia) na Richard Shaba baada ya mazungumzo yao yaliyofanyika Ikulu Dar es Salaam Septemba 15, 2014. Picha na OMR