Tuesday, September 30, 2014

KUTOKA BUNGE LA KATIBA MJINI DODOMA LEO



KUTOKA BUNGE LA KATIBA MJINI DODOMA LEO
Wahudumu wa Bunge wakibeba masanduku ya kura ili kuyapeleka kwenye chaumba cha kuhesabia kura baada ya wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba kumaliza kazi ya kupiga kura Septemba 30, 2014.
Wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na Waziri wa Ardhi , Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka wakiteta bungeni Mjini Dodoma Septemba 30, 2014. Kushoto ni Spika wa Bunge, Anne Makinda.
 Wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na Kingunge Ngombale Mwiru (kulia) wakizungumza na Mama Loyce Samike, Mama mzazi wa Mjumbe wa Bunge hilo, Dkt. Angelina Samike (wapili kushoto) kwenye viwanja vya Bunge mjini Dodoma Septemba 30, 2014. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)