Wednesday, September 17, 2014

Costa Siboka aendelea na ziara yake kanda ya ziwa




Costa Siboka aendelea na ziara yake kanda ya ziwa
Mfalme wa nyimbo za asili nchini Tanzania Costa Siboka, Baada ya kufanya kufuru na kuvunja Rekodi katika Miji ya Mwanza, Geita,Visiwa vya Ghana na Ukerewe Sasa anatarajia kumalizia ziara yake katika Miji ya Bunda,Bariadi,Shirati,Tarime , Butiama na Dutwa.Shoo hizo zitafanyika tarehe 22 Septemba 2014 mpaka tarehe 30 septemba 2014.Mfalme Siboka akiwa na kundi lake ametamba na kusema yeye in jeshi la Mtu mmoja...Hakunaga shiiida, Vuta raha Barimi tumpokee Mfalme.Siboka yupo katika utambulisho WA nyimbo yake mpya Engele yange aliouimba kwa lugha za makabila manne.Kisukuma,Kihaya,Kikerewe,Kijita na Kikurya.