Wednesday, August 20, 2014

VODACOM YATOA MADA KUHUSIANA NA HUDUMA ZAKE KWENYE WARSHA YA KUSHIRIKISHANA NJIA ZA KUBORESHA NA KUPANUA HUDUMA ZA KIFEDHA



VODACOM YATOA MADA KUHUSIANA NA HUDUMA ZAKE KWENYE WARSHA YA KUSHIRIKISHANA NJIA ZA KUBORESHA NA KUPANUA HUDUMA ZA KIFEDHA
 
 Mkuu wa Idara ya Masoko na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania ,Kelvin Twissa akitoa mada juu ya huduma zinazotolewa na kampuni yake wakati wa Warsha ya kushirikishana uzoefu kuhusu njia za kuboresha na kupanua huduma za kifedha kwa biashara ndogo na za kati hapo jana. Warsha hiyo iliandaliwa na Tanzania Private Sector Foundation (TPSF) na kudhaminiwa na Vodacom.Kushoto ni muongozaji  wa mada Felix Mlaki  na Katikati ni Mtaalamu toka Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE)Moreme Marwa. 
 Mmoja wa washiriki wa Warsha ya kushirikishana uzoefu kuhusiana na njia za kuboresha na kupanua huduma za kifedha kwa biashara ndogo na za kati iliyoandaliwa na Tanzania Private Sector Foundation (TPSF) na kudhaminiwa na Vodacom Tanzania, akisoma moja ya jarida la Vodacom  wakati wa warsha hiyo iliyofanyika kwenye hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam hapo jana. 
Baadhi ya washiriki wa Warsha ya kushirikishana uzoefu kuhusu njia za kuboresha na kupanua huduma za kifedha kwa biashara ndogo na za kati iliyoandaliwa na Tanzania Private Sector Foundation (TPSF) na kudhaminiwa na Vodacom Tanzania,wakifuatilia mada kwa makini  zilizokuwa zikitolewa  wakati wa  warsha hiyo iliyofanyika kwenye hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam hapo jana.