Saturday, July 12, 2014

MWIGULU NCHEMBA ALONGA UMOJA WA MATAIFA



MWIGULU NCHEMBA ALONGA UMOJA WA MATAIFA
 Naibu Waziri wa  Fedha wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.  Mwigulu Nchemba ( Mb) akizungumza wakati wa majadiliano kuhusu masuala ya  Ushirikiano wa Kimaendeleo uliofanyika kwa siku mbili hapa Umoja wa Mataifa. Mhe. Naibu  Waziri  alikuwa mmoja wa wanajopo wanne walioendesha majadiliano hayo. Katika mchango wake, Naibu  Waziri pamoja na mambo mengine amesisitiza  kuwa  Ushirikiano wa Kimaendeleo bado  una mchango mkubwa katika ufanikishaji wa  suala zima la maendeleo endelevu lakini akataka   iwemo mifumo ya ufuatiliaji ambayo  itakuwa jumuishi.
 Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Balozi Tuvako Manongi ambaye alifuatana na  Mhe. Naibu Waziri katika  mkutano huo. Aliyeketi nyuma ya Balozi  Manongi, ni  Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiwano wa Kimataifa, Balozi Celestin Mush na  pembeni ya  Balozi ni msaidizi wa Naibu Waziri.
 Ujumbe wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambao kwa takribani wiki mbili umekuwa ukihudhuria na kushiriki mikutano na mijadala  mbalimbali  inayohusu mwelekeo wa  ukamilishwaji wa  malengo ya maendeleo ya milenia ( MDGs), mchakato wa  maandalizi ya ajenda  na malengo mapya ya maendeleo endelevu baada ya 2015 na Ushirikiano wa Kimaendeleo. Mikutano  hiyo   imeandaliwa  na Balaza la Umoja wa Mataifa linalohusika na masuala  ya Uchumi na Maendeleo ya Jamii  ( ECOSOC)
 Sehemu ya  washiriki waliokuwa wakifuatilia majadiliano hayo na ambapo  baada ya wanajapo kutoka mchango wao walipata fursa ya  kuuliza maswali au kuchangia maoni yao. Mkutano huu wa siku mbili kuhusu Ushirikiano wa Kimaendelea umefanyika  nchi na mwamvuli wa  ECOSOC 
 wajumbe walioshiriki majadiliano kuhusu Ushirikiano wa Kimaendeleo  wakifuatilia majadiliano hayo.