Friday, July 18, 2014

MICHAEL CARRICK KIMEO …NJE YA UWANJA KWA MIEZI MITATU …afanyiwa upasuaji wa enka


MICHAEL CARRICK KIMEO …NJE YA UWANJA KWA MIEZI MITATU …afanyiwa upasuaji wa enka

I've had better days! Michael Carrick posted this                    picture on his Instagram as it was announced he'll be                    out for 10 weeks with damaged ankle ligaments

MICHAEL Carrick ameumia enka na atakuwa nje ya uwanja kwa wiki 10 hadi 12, kocha mpya wa Manchester United Louis van Gaal amefichua.

Kiungo huyo mwenye umri wa miaka 32 alifanyiwa upasuaji Alhamisi asubuhi na sasa atakosa mwanzo wa kampeni za msimu ujao.

Louis van Gaal amesema hilo ni pigo kwa kikosi chake kwa vile Michael Carrick ni mchezaji mzoefu.

"Siku zote ni muhimu kuwa na wachezaji wazoefu, lakini sio kwa umri tu, sio kwa uzoefu wa soka tu, bali pia kwa uzoefu wa mambo ya kibinadamu," alisema Van Gaal.

Taarifa rasmi ya klabu imesema: "Michael Carrick amefanyiwa upasuaji wa enka yake ya kushoto na atakuwa nje ya uwanja kwa wiki 10 hadi 12."