Friday, November 02, 2012

KAMERA YA MTAA KWA MTAA JIJINI MWANZA IKIANGAZIA USAFI WA JIJI HILO.



Hapa ni katikati ya jiji pakiwa na bustani zinazovutia Mbele ya Mtaa Kemondo ikilipamba jiji hilo.


Kama majiji yote yangekuwa na vifaa kama hivi kila kwenye nguzi ya taa kama ilivyo jijini Mwanza basi suala la usafi wa Mazingira kwenye majiji yetu lingekuwa lakujivunio kuliko ilivyo sasa.


Hata mtu anaefanya usafi mwenyewe hufanana na usafi husika tofauti kabisa na majiji mengine huyo anaefanya usafi mwenyewe mchafu kweli atafanya usafi? Ipo haja ya majiji mengine kuja kujifunza haya.


Kamera yatu ilifika hadi kwenye eneo la Soko kuu na kukuta gari la kisasa la kuzolea taka likiendelea na kazi na kwamujibu wa watu walizozungumza na MTAA KWA MTAA, kazi hiyo hufanywa kila siku. Kama ilivyo kwa jiji la Dar es Salaam wafanyabiashara hupanga biashara zao hadi sehemu za takatata hizi ni baadhi ya Changamoto zinazotakiwa kufanyiwa kazi.