Wednesday, September 19, 2012

Spika Makinda Ashiriki Msiba Wa Baba Yake Mhe. Tundu Lissu



Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda akimfariji Mbunge wa Singida Mashariki Mhe. Tundu Lissu alipofika kuhani msiba wa Marehemu baba yake Mhe. Tundu Lissu mzee Agustinio Lissu Mughwai Nyumbani kwake tegeta, Dar es Salaam. Mzee Lissu alifariki Jumapili tarehe 16 Septemba, 2012, katika Hospitali ya Muhimbili, Dar es salaam na anatarajiwa kuzikwa jumamosi Singida
 
Spika wa Bunge akisaini kitabu cha maombolezo  

Mhe. Spika akimfariji mbunge wa Viti maalum Chadema
Mhe. Christina Lissu ambaye pia ni dada yake na Mhe. Tundu Lissu alipowatembelea kuhani msiba wa baba yao Tegeta

 
Mbunge wa Singida Mjini Mhe. Tundu Lissu akiteta jambo na Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda alipofika kuhani msiba wa baba yake Mhe. Lissu Mzee Agustinio Lissu Mughwai Tegeta Dar es Salaam
Picha zote na Owen Mwandumbya wa Bunge


PATAKAZI.NET (MIHANGAIKO) BLOG INAUNGANA NA FAMILIA YA LISSU 

KATIKA KIPINDI HIKI KIGUMU BWANA AMETOA BWANA 

AMETWAA JINA LAKE LIHIMIDIWE