Sunday, September 30, 2012

NATHAN ATOA ZAWADI KWA WATOTO WANAOUMWA UGONJWA WA SARATANI


  Mchora vibonzo, Nathan Mpangala, akitoa maelekezo ya jinsi ya kuchora vibonzo kwa baadhi ya watoto wanaoendelea na matibabu ya saratani katika Hospitali ya Taifa Muhimbil, Jijini Dar es Salaam, Jumamosi, 29.09.2012. Ziara hiyo ni sehemu ya maadhimisho miaka sita ya KIBONZO kinachorushwa ITV na pia ni sehemu ya shughuli za kijamii ya Tuzo ya Mchora Katuni Bora wa 2011, aliyopewa na Baraza la Habari Tanzania, (MCT).
 Mchora katuni wa gazeti la Tanzania Daima, Said Michael, aliyechutama, akiwaelekeza baadhi ya watoto wanaosumbuliwa na saratani jinsi ya kuchora katuni katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, Dar es Salaam, jana. (29.09.2012). Said, alikuwa miongoni mwa wachoraji katuni waliungana kumsindikiza mchoraji mwenzao, Nathan Mpangala, aliyekwenda kutembelea watoto hao ili kuwapa zawadi na kuchora nao ikiwa maadhimisho miaka sita ya KIBONZO kinachorushwa ITV na pia ni sehemu ya shughuli za kijamii baada ya kupata tuzo ya uchoraji bora wa katuni, 2011 aliyopewa na Baraza la Habari Tanzania, (MCT).