Friday, September 21, 2012

Mkutano Wa Katibu Mkuu Wizara Ya Mambo Ya Ndani Ya Nchi Na Wanamichezo


Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi,  Mwamini Malemi akiwapa nasaha wanamichezo (hawapo pichani) wa wizara hiyo katika tafrija fupi ya kuwaaga wawakilishi hao wa wizara ambao watashiriki katika mashindano ya Shirikisho ya Michezo ya Wizara na Idara za Serikali (Shimiwi) yanayotarajiwa kuanza mjini Morogoro kesho. Kulia ni Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Mbarak Abdulwakil pamoja na Mwenyekiti wa Michezo, Juma Katanga.



  • Wanamichezo wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi wakiifurahia nasaha za viongozi wa wizara hiyo (hawapo pichani) katika tafrija fupi ya kuwagwa wanamichezo hao ambao wanasafiri leo kuelekea mjini Morogoro katika mashindano ya Shirikisho ya Michezo ya Wizara na Idara za Serikali (Shimiwi) yatakayoanza rasmi mjini humo kesho

  • Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak Abdulwakil akiwapa nasaha wanamichezo (hawapo pichani) wa wizara hiyo katika tafrija fupi ya kuwaaga wawakilishi wa wizara hiyo ambao watashiriki katika mashindano ya Shirikisho ya Michezo ya Wizara na Idara za Serikali (Shimiwi) iliyofanyika wizarani hapo jijini Dar es Salaam leo. Mashindano hayo yanayotarajiwa kuanza mjini Morogoro kesho. Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Mwamini Malemi pamoja na Katibu wa Michezo, Jarahi Kilemile.
    IMEANDALIWA NA KITENGO CHA MAWASILIANO YA SERIKALI WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI. 21 DISEMBA, 2012.
    0754 777478, 0714 809480.